Arusha
Home » » Kijana aliyetoka Dar hadi Arusha kwa baiskeli amezindua rasmi kitabu chake

Kijana aliyetoka Dar hadi Arusha kwa baiskeli amezindua rasmi kitabu chake

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mheshimiwa Nabii Mkuu Dr GeorDavie Royal Mkuu ,   jana amezindua rasmi kitabu cha " KUKIWA NA FOLENI" kilichoandikwa na Wiseman Luvanda.
Pia Nabii Dr.GeorDavie alimpongeza kwa kitendo chake  alichoamua kufanya kwa kuwa balozi wa barabarani  kwa kutoka Jijini Dar es salaam hadi mkaoni Arusha wa usafiri wa baiskeli
Akizungumza na wadau waliohudhuria hafla hiyo mtunzi wa kitabu hicho alisema vijana wanapaswa kutumia vipaji vyao kwa kujituma, kuthubutu na kufanya kazi kwa nguvu  na si kulalamika kila siku,  jambo linalopelekea kuibuka kwa makundi mbalimbali kama vile Panya Road na mengineyo.
Aidha mwandishi huyo amewataka wadau mbalimbali kumuunga mkono katika kukinunua kitabu hicho cha " KUKIWA NA FOLENI" , ambacho pia amekiandika kwa lugha ya Kiswahili  ili kuweza kukisambaza nchi nzima.
Tazama baadhi ya picha za tukio hili hapo chini
Pichani ni Mwandishi wa kitabu hicho Wiseman Luvanda, Akizungumza na baadhi ya wadau waliohudhuria kongamano hilo jana Jijini Arusha. Picha na msumbanews blog
Nabii Mkuu Dr GeorDavie Royal Mkuu akipokea kitabu kutoka kwa Mwandishi Wiseman Luvanda.Picha na msumbanews blog
Baadhi ya wadau mbali waliojitokeza kwenye kongamano  la kuinuliwa viwango na uzinduzi wa kitabu hicho.Picha na msumbanews blog
Mwandishi Wiseman Luvanda akifuatilia kwa makini kongamano la kuinuliwa viwango ambalo lilifuatana na uzinduzi wa kitabu chake.Picha na msumbanews blog

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa