Arusha
Home » » SERIKALI KUGHARIMIA MAZISHI YA WANAFUNZI 33 WALIOFARIKI KWENYE AJALI; MBUNGE LEMA ATOA SALAMA ZA RAMBIRAMBI

SERIKALI KUGHARIMIA MAZISHI YA WANAFUNZI 33 WALIOFARIKI KWENYE AJALI; MBUNGE LEMA ATOA SALAMA ZA RAMBIRAMBI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Shule ya Lucky Vincent

SERIKALI ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania itagharamia shughuli za mazishi ya wanafunzi 33, walimu wawili na dereva mmoja waliopoteza maisha kwenye ajali ya basi iliyotokea kwenye kata ya Rothia baada ya kutumbukia kwenye korongo la mto Malera.
Kwa mujibu wa Meya wa jiji la Arusha, Mhe. Calist Lazaro amesema gharama hizo ni pamoja na kununua sanda pamoja na majeneza.
Meya wa Arusha, Calis Lazaro
Akitoa taarifa hiyo leo Mei 7, 2017, Meya huyo alisema kuwa taarifa za awali zinaonyesha kuwa tayari Serikali imekwishalipia gharama za majeneza na sanda ya kuhifadhia miili ya marehemu ambapo kesho kwenye uwanja wa kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid, patafanyika ibada ya kuaga miili ya mareghemu.
SHULE YAFUNGWA
Shule ya Lucky Vicent imefungwa kwa siku saba kufuatia vifo vya wanafunzi wake 33, Walimu wawili na dereva mmoja vilivyotokea kwenye ajali ya gari Juma wilayani Karatu, mkoani Arusha.
Mbunge wa Arusha, Mhe.Godbles Lema
Kutokana na ajali hiyo Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema na wabunge wengine wa Chadema wamefika shuleni hapo kutoa pole.
Lema kwa niaba ya wabunge wenzake ameeleza kusikitishwa na msiba huu na amewapa pole wafiwa lakini akatoa angalizo kusiingizwe siasa katika msiba huu mkubwa.
Meya wa jiji la Arusha Mstahiki Calist Lazaro ameeleza kuwa Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, Waziri wa Tamisemi, George Simbachawene na Waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichakowalitarajiwa uwasili jioni hii ya Jumapili Mei 7, 2017 ili kuzungumza na jumuiya ya wshule ikiwa ni pamoja na wafiwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ataongoza watanzania kwenye ibada ya kuaga miili ya marehemu hao kwenye uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid jijini Arusha kuanzia saa 3 asubuhi, hii ni kwa mujibu wa taarifa ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Mrisho Gambo.
Mkuu wa shule hiyo, Ephraem Jackson amesema hadi sasa vifo ni 36 na wanafunzi wawili bado wamelazwa Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru. Wanafunzi hao ni Sadiely Ismail na Wilson Tarimo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa