RAIS SAMIA ATAJWA KINARA AFYA YA MSINGI

 


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametambuliwa kuwa kinara katika kuimarisha huduma za afya ya msingi kutokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana nchini, hususan katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto.
Akifungua Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Aya ya Msingi (IPHC) kwa niaba ya Rais Samia katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Jijini Arusha (AICC), Septemba 9, 2026, Waziri Mkuu amesema mafanikio hayo yameiwezesha Tanzania kutambulika kimataifa, ikiwemo Rais Samia kutunukiwa Goalkeeper Award mwaka 2025 na kuteuliwa kuwa kinara wa Umoja wa Afrika wa huduma za afya ya mama na mtoto mwaka 2026.

Rais Mhe. Dkt. Samia awasili Mkoani Arusha kwa ajili ya kushiriki katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA. Amos Makalla mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), tarehe 06 Machi, 2026. Rais Mhe. Dkt. Samia amewasili Jijini Arusha kwa ajili ya kushiriki katika Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) utakaofanyika tarehe 07 Machi, 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) tarehe 06 Machi, 2026. Rais Mhe. Dkt. Samia amewasili Jijini Arusha kwa ajili ya kushiriki katika Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) utakaofanyika leo tarehe 07 Machi, 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC).

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiangalia Kikundi cha Sanaa cha Maasarie Troupe mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) tarehe 06 Machi, 2026. Rais Mhe. Dkt. Samia amewasili Jijini Arusha kwa ajili ya kushiriki katika Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)unaotarajiwa kufanyika tarehe 07 Machi, 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC). 

 






Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

NSSF YAIBUKA MSHINDI WA KWANZA NA KUPOKEA TUZO KWA UZINGATIAJI WA SHERIA YA SERIKALI MTANDAO, VIWANGO NA MIONGOZO



Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umeibuka mshindi wa kwanza na kutunukiwa tuzo kwa
Taasisi zilizofanya vizuri katika uzingatiaji wa Sheria ya Serikali Mtandao, viwango na miongozo kwa taasisi zilizo katika ngazi ya nne ya ukomavu wa TEHAMA Serikalini.

Tuzo hiyo ilitolewa na Ridhiwani Kikwete, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, na kupokelewa na Bw. Donald Mhaiki, Mkurugenzi wa TEHAMA wa NSSF.

Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ilifanyika wakati wa kilele cha Kikao cha 6 cha Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), kilichofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha International Conference Centre (AICC), jijini Arusha.

Ushindi huo unaonesha jitihada za NSSF katika kuimarisha matumizi ya TEHAMA na kuzingatia kikamilifu sheria, viwango na miongozo ya Serikali Mtandao nchini.

Serikali yazindua Sera ya Taifa ya Kinga ya Jamii na ‘Hifadhi Scheme’ kwa Waliojiajiri

Serikali yazindua Sera ya Taifa ya Kinga ya Jamii na ‘Hifadhi Scheme’ kwa Waliojiajiri

Na MWANDISHI WETU, 
ARUSHA. Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano imezindua Sera ya Taifa ya Kinga ya Jamii pamoja na Mpango wa Hifadhi ya Jamii kwa Wananchi Waliojiajiri ‘Hifadhi Scheme’ hatua inayolenga kupanua wigo wa hifadhi ya jamii na kuongeza ushirikishwaji wa wananchi katika mifumo ya kinga ya kijamii.

Uzinduzi huo umefanyika Februari 9, 2026 katika mkutano wa wadau wa sekta ya kinga ya jamii uliofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC), ukiongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu kwa niaba ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Sangu alisema sera hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, inayolenga kuhakikisha wananchi wanapata huduma jumuishi za hifadhi ya jamii. Aliongeza kuwa tangu 2018, Serikali imefanya maboresho ikiwemo kuunganisha Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na kubaki na NSSF na PSSSF ili kuongeza ufanisi wa huduma na ulipaji wa mafao.

Mhe. Sangu alisema maboresho hayo yameongeza idadi ya wanachama. NSSF imeongezeka kutoka wanachama 808,935 mwaka 2020 hadi zaidi ya wanachama 2,213,659 mwaka 2025, huku PSSSF ikiongezeka kutoka 697,677 hadi 899,948. Aidha, thamani ya uwekezaji wa Mifuko imeongezeka kutoka shilingi trilioni 9.36 hadi trilioni 20.14, na jumla ya thamani ya Mifuko kufikia trilioni 24.20.

Kuhusu mpango wa Hifadhi Scheme, alisema hadi Desemba 2025 zaidi ya wanachama 500,000 kutoka makundi mbalimbali yakiwemo wakulima, wafugaji, wavuvi na wajasiriamali wamejiunga, huku lengo likiwa kufikia wanachama milioni 5.5 ifikapo Juni 2031.

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Mary Maganga, alisema Serikali imeipa NSSF jukumu la kupanua wigo wa hifadhi ya jamii kwa wananchi waliojiajiri ili kuhakikisha sera mpya inaleta matokeo yanayotarajiwa.

Awali, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba, alisema Mfuko unaendelea kuboresha utoaji wa huduma, kuongeza uandikishaji wa wanachama wapya, na kupanua wigo wa uwekezaji ndani na nje ya nchi, ikiwemo nchi za SADC na Afrika Mashariki.

Bw. Mshomba alisema Mfuko umepata mafanikio makubwa katika Serikali ya awamu ya sita ambapo thamani ya NSSF imeongezeka kutoka trilioni 4.8 mwaka 2021 hadi trilioni 10.4 Desemba 2025, na kuwa imepata ziada kwa miaka minne mfululizo kuanzia 2021 hadi mwaka wa fedha 2024/25, ikivuka lengo la ziada ya shilingi trilioni moja.

Akizungumzia ukusanyaji wa michango, Bw. Mshomba alisema Mfuko umeendelea kuvuka malengo, ambapo mwaka wa fedha 2023/24 ulifikia zaidi ya shilingi trilioni mbili, huku mwaka 2024/25 makusanyo yakizidi trilioni 2.4 na kwamba katika kipindi cha miaka mitano mfululizo kuanzia 2020 hadi 2025, NSSF imefanikiwa kuvuka lengo la kukusanya angalau shilingi trilioni moja kwa mwaka. 

Bw. Mshomba aliongeza kuwa mafanikio hayo yamechangiwa na juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. NSSF ina zaidi ya wanachama milioni 2.3 na imejikita kuboresha huduma kupitia TEHAMA na mpango wa miaka mitano unaolenga kufanikisha malengo ya Dira ya Taifa 2050 na Ilani ya Uchaguzi ya CCM. 




 

TAARIFA KWA UMMA - ZOEZI LA UHAKIKI WA WASTAAFU NA WATEGEMEZI

 TAARIFA KWA UMMA - ZOEZI LA UHAKIKI WA WASTAAFU NA WATEGEMEZI


 

DC MTATIRO ATUNUKIWA SHAHADA YA SABA! APATA UZAMILI WA MASOMO YA AMANI NA USALAMA

 


Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro, ni miongoni mwa wahitimu waliotunukiwa shahada za uzamili katika mahafali yaliyofanyika Ijumaa, Februari 6, 2026, katika Chuo Kikuu cha Uhasibu Arusha (IAA), yaliyofanyika Ngurdoto jijini Arusha.

Katika mahafali hayo, Mtatiro ametunukiwa Shahada ya Uzamili ya Masomo ya Amani na Usalama (Master of Arts in Peace and Security Studies) na kuchaguliwa kuwa msemaji mkuu wa wahitimu wote, ambapo alitoa hotuba kwa niaba yao.

Amesisitiza umuhimu wa vijana kuendelea kujifunza na kujiongezea maarifa kulingana na nafasi na ndoto zao, akieleza kuwa elimu hiyo inapaswa kuendana na mahitaji ya ujuzi, ushindani wa kimataifa pamoja na vipaumbele vya kimkakati vya maendeleo ya Tanzania ya sasa.

Mbali na shahada hiyo mpya ya uzamili, Mtatiro pia anamiliki Stashahada ya Uzamili ya Sheria kwa Vitendo (Postgraduate Diploma in Legal Practice) pamoja na shahada nyingine tatu za uzamili ambazo ni: Uzamili wa Usimamizi wa Umma Uzamili wa Sera za Umma na Uzamili wa Mawasiliano ya Umma.

Aidha, ana shahada mbili za kwanza ambazo ni:vShahada ya Sanaa katika Elimu na Shahada ya Sheria (LL.B).

Historia ya Uongozi wa Wanafunzi

Akiwa mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Mtatiro anakumbukwa kwa mchango wake katika harakati za wanafunzi zilizoleta mabadiliko katika usimamizi wa sera za elimu ya juu, hususan eneo la mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.

Katika kipindi hicho, aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali za uongozi wa wanafunzi zikiwemo: Waziri wa Mikopo – DARUSO. Waziri Mkuu – DARUSO na Katibu Mkuu – TAHLISO.

Uzoefu wa Kisiasa na Kitaifa

Mtatiro pia aliwahi kuwa kiongozi mwandamizi wa Chama cha Wananchi (CUF) kati ya mwaka 2009 na 2017, akihudumu katika nafasi mbalimbali zikiwemo: Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Sheria. Naibu Katibu Mkuu – CUF Tanzania Bara na Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi wa Taifa.

Vilevile, aliwahi kuwa Mjumbe wa Bunge la Katiba kwa kuteuliwa na Rais wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.

Uongozi Serikalini

Kwa upande wa utumishi wa umma, Mtatiro aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru mwaka 2019, nafasi aliyohudumu hadi mwaka 2024. Kuanzia mwaka 2024 hadi sasa anahudumu kama Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga.

Mbali na majukumu ya kiutawala, Mtatiro anatambulika pia kama mwalimu, wakili, na mchambuzi wa sera za umma mwenye uzoefu mpana katika masuala ya utawala na maendeleo.



MAKALLA AIPONGEZA SERIKALI, JKCI YATOA VIPIMO BURE MAGONJWA YA MOYO ARUSHA


Na Pamela Mollel,Arusha 

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla, amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuimarisha huduma za afya kwa kusogeza huduma za kibingwa za magonjwa ya moyo karibu na wananchi.

 Anasema uanzishwaji wa Kituo cha Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) katika Hospitali ya Arusha Lutheran Centre (Seliani) utawanufaisha wananchi wa Arusha na mikoa ya jirani, pamoja na watalii na wageni watakaoshiriki michuano ya AFCON 2027.

Mhe Makalla anayasema hayo wakati wa ziara yake ya kukagua zoezi la utoaji wa vipimo na matibabu ya magonjwa ya moyo bure, ambapo jumla ya wananchi takribani 1,200 wamenufaika na huduma hizo, huku Serikali ikiahidi kuwawezesha wananchi wasiokuwa na uwezo wanaohitaji rufaa ili wapate matibabu zaidi katika Taasisi ya Moyo ya JKCI jijini Dar es Salaam. 

Aidha, amewahamasisha wananchi kujiunga na Bima ya Afya kwa Wote ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wakati.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge, amesema katika Kanda ya Kaskazini, magonjwa ya moyo na magonjwa yasiyoambukiza yameendelea kuonekana kwa kasi, ambapo kupitia programu ya upimaji wa afya, zaidi ya wananchi 3,000 wamejitokeza kupima afya zao. 

Anasema kuwa kati yao, asilimia 9 walibainika kuwa na matatizo ya moyo, huku asilimia 29 wakigundulika kuwa na shinikizo la damu, ugonjwa uliokuwa unaongoza zaidi kwa wananchi wenye umri kati ya miaka 45 hadi 80

Dkt. Kisenge ameongeza kuwa sababu kuu zinazosababisha ongezeko la magonjwa hayo ni kutofanya mazoezi ya mwili, unene uliopitiliza, unywaji wa pombe kupita kiasi, uvutaji wa sigara, pamoja na kutokuzingatia lishe bora, akiwahimiza wananchi kubadili mtindo wa maisha na kufanya uchunguzi wa afya mara kwa mara ili kuepuka madhara makubwa ya kiafya.





 

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

UNESCO Yaunga Mkono Juhudi za Serikali Kuboresha Mfumo wa Usimamizi wa Mafunzo Endelevu ya Walimu (MEWAKA)

Picture1

Picture2

Picture3

Picture4

Picture5

Na Mwandishi Wetu, Arusha.

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeonyesha dhamira ya dhati Kufanya kazi bega kwa bega na wadau wa maendeleo kuhakikisha uboreshaji wa mfumo wa usimamizi wa mafunzo endelevu wa walimu kazini yaani MEWAKA unaboreshwa na kukamilika kwa wakati na kwa ufanisi ili kuwezesha mahitaji ya walimu wa Sekondari.

Akizungumza wakati wa kuhitimisha warsha  iliyofanyika kwa muda ya siku mbili ya tarehe 28 na 29 Agosti 2025, ya mapitio ya mfumo wa MEWAKA ulioboreshwa Mratibu wa Mradi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bi. Lina Rujweka, alitoa shukrani kwa juhudi na muda uliowekezwa na wadau wote, ikitambua mchango wao muhimu unaotarajiwa kuleta mafanikio makubwa katika utekelezaji wa mradi huu hasa UNESCO na Jamhuri ya Korea kupitia mradi wa ‘’KFIT III wa Transforming Education through ICT in Africa’’ kwa kuendelea kutoa msaada wa kifedha.

Shirika la UNESCO Dar es Salaam, kwa kushirikiana na Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), inaendelea na juhudi za uboreshaji mfumo wa MEWAKA ili kuzingatia mahitaji ya walimu wa shule za sekondari.

Ushirikiano huu ulitokana na tathmini ya mahitaji iliyoonyesha kuwa mfumo wa sasa ulikuwa umeundwa mahsusi kwa ajili ya kuwa jukwaa la mafunzo ya maendeleo ya kitaaluma kwa walimu wa shule za msingi.

Hivyo, wadau walikutanishwa ili kupitia toleo la awali la mfumo wa MEWAKA kwa lengo la kuhakikisha umuhimu, ubora, na uendelevu wa muda mrefu wa jukwaa hilo.

Wadau hao walikuwa kutoka  wizara ya elimu, sayansi na Teknolojia , Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Taasisi ya Elimu Tanzania, Tume ya Kitaifa ya UNESCO na baadhi ya walimu wa shule za sekondari.

Katika hotuba yake ya ufunguzi, mwakilishi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Ally Mape alisema majukwaa ya kidijitali ni nyenzo yenye nguvu ya maendeleo ya kitaaluma, yanayochangia kwa kiasi kikubwa kuwawezesha walimu kupata ujuzi na kujiamini ili kufanikisha kazi zao katika Dunia ya sasa.

Kwa upande wake mkuu wa Sekta ya Elimu kutoka Ofisi ya UNESCO Dar es Salaam, Dkt. Faith Shayo, ameeleza kuwa lengo kuu ni kupanua upatikanaji wa mafunzo endelevu ya kitaaluma kupitia majukwaa ya kidijitali, hivyo itasaidia kuboresha matokeo ya ufundishaji na ujifunzaji kote nchini.

Hata hivyo Dkt. Shayo aliwahimiza wadau kutoa maoni na mitazamo yao kusaidia kuhakikisha toleo la mwisho la mfumo huu sio tu kuwa la kisasa bali pia rahisi kutumia na lenye matokeo chanya.

Mpango huu unalingana na juhudi za Serikali za kuunganisha TEHAMA katika elimu, kama inavyoonekana katika sera na mikakati muhimu ya kitaifa ikiwemo Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 toleo la 2023, Mkakati wa Kitaifa wa Elimu ya Kidijitali 2025 – 2030, Dira ya Maendeleo ya 2050, Mitaala ya Elimu ya Msingi na ya Ualimu, pamoja na mipango ya kimataifa kama vile Malengo ya Maendeleo Endelevu hasa lengo namba nne.


Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa