Arusha
Home » » WASIMAMISHWA KAZI NA MKUU WA MKOA WA ARUSHA MH. MRISHO GAMBO

WASIMAMISHWA KAZI NA MKUU WA MKOA WA ARUSHA MH. MRISHO GAMBO

 Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mrisho Mashaka Gambo, amewasimamisha kazi watumishi watatu wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro kwa tuhuma za ubadhilifu wa fedha za uchaguzi wa mwaka 2015.
Baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Ngorongoro, wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa Mrisho Gambo(hayupo pichani),alipokuwa akitoa taarifa ya kamati ya uchunguzi aliyoiunda kuchunguza mapato na matumizi katika halmashauri hiyo.


Watumishi hao ni pamoja na Bi. Hadija Mkumbwa ambae alikuwa msimamizi wa uchaguzi wa mwaka 2015 na kumfuta cheo hicho,bwana Evansi Mwalukasa alikuwa mwekahazina wa halmashauri na  bwana Sembeli Sinayo yeye alikuwa mwanasheria wa halmashauri.

Maamuzi hayo yamefikia baada yakubainika kuna upotevu  wa fedha za uchagu takribani Milioni 188 ambazo matumizi yake hayakuwekwa  wazi na pia Milioni 20 zilitumika kwa manunuzi ambayo hayakufuata taratibu za manunuzi ya serikali.

“Kuanzi sasa nawasimamisha  kazi hawa watumishi watatu kwasababu wameisababishia serikali hasara ya takribani Milioni 128 ambazo zilikuwa fedha za uchaguzi”.

Aidha Muheshimiwa Gambo alisema maamuzi hayo yametokana na taarifa aliyokabidhiwa na kamati aliyoiunda yakuchunguza mapato na matumizi ya fedha za halmashauri hiyo na kubaini upotevu huo wa fedha nyingi ambazo zingeweza kusaidia shughuli mbalimbali za uchaguzi katika Wilaya hiyo.

Ambapo fedha nyingine zimetumika kwenye manunuzi ambayo hayakufuata taratibu na sheria za manunuzi ya serikali ,hivyo ni kinyume kabisa na taratibu za serikali katika maswala ya manunuzi.

Akisisitiza kwa watumishi wa serikali kufuata taratibu, sheria na kanuni mbalimbali katika kutekeleza majukumu yao ili kuepuka migongano na uvunjifu wa sheria mahala pa kazi nakupelekea kupoteza kazi  zao.
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa