Arusha
Home » » MKUU WA MKOA WA ARUSHA MH. MRISHO GAMBO APOKEA MSAADA WA SIMENTI NA MABATI KUTOKA HANIL JV

MKUU WA MKOA WA ARUSHA MH. MRISHO GAMBO APOKEA MSAADA WA SIMENTI NA MABATI KUTOKA HANIL JV

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mrisho Mashaka Gambo amepokea mifuko 500 ya simenti na mabati 500 kutoka kwa kampuni ya ukandarasi ya Hanil JV Jiangsu kutoka Korea inayojenga barabara ya Tengeru Sakina.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo akitoa shukrani kwa kampuni ya ukandarasi ya Hanil JV Jiangsu kwa kutoa msaada wa mifuko ya simenti 500 na mabati ya 500 kwa shughuli za maendeleo za Mkoa wa Arusha.
 
 
Msaada huo umetolewa ofisini kwake ambapo tukio hilo limeweza kushuhudiwa na viongozi mbalimbali wa Mkoa,Wilaya na Wabunge wa viti maalumu wa Mkoa wa Arusha.
Akipokea msaada huo,Mrisho Gambo amesema atagawa mifuko 100 ya simenti na mabati 100 kwaajili ya ujenzi wa Zahanati kata ya Murieti kwasababu kumekuwa na ongezeko kubwa sana la wagonjwa katika hospitali ya Mkoa Mt.Meru wanaotoka maeneo hayo hivyo ujenzi huo utasaidia  kupunguza wagonjwa katika hospitali hiyo.
Pia yatakayo baki atayapeleka Wilaya ya Longido katika kusaidia ujenzi wa bweni la shule ya sekondari Longido ambayo liliungua moto nakuteketeza kila kitu.
 
“Napenda kuishukuru na kuipotengeza kampuni ya ukandarasi ya barabara ya Tengure Sakina na ile ya njia mbadala(by path) kwakutoa msaada huu na kwakuwa tumeshaanza  mkakati wa ujenzi wa madara kwa shule za msingi na Sekondari,hivyo nitagawa hayo mifuko ya simenti 100 na mabati 100 ikajenge Zahanati kata ya Murieti na yaliyobaki yataenda Longido katika ujenzi wa bweni lililoungua”.
 
Mkurugenzi  Mtendaji wa kampuni ya ukandarasi ya Hanil JV Jiangsu bwana Xie Jianbao amesema kampuni yao imetoa msaada huo ikiwa ni moja ya shughuli zao zakusaidia jamii katika shughuli mbalimbali za maendeleo.
“Tumetoa mifuko ya simenti 500 na mabati 500 kama moja ya mchango wetu katika kusaidia jamii yetu kwenye shughuli mbalimbali za maendeleo”.
Aidha Mkurungezi wa Jiji la Arusha,Athumani Kihamia alisema  kutokana na wingi wa wananchi waliopo katika kata ya Murieti Zahanati hiyo itaenda kuwasaidia sana na kwakipindi kisichozidi miezi 2 Zahanati hiyo itakamilika na wananchi wataweza kuitumia.
Ukosefu wa kituo cha afya katika kata ya Muriet ulibainika baada ya Mkuu wa Mkoa Gambo kufanya ziara katika kata hiyo nakupata malalamiko kutoka kwa wananchi kuwa wanatembe umbali mrefu sana kutafuata huduma za afya.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa