Arusha
Home » » KONDOM MPYA ZINAZOITWA ZANA ZAZINDULIWA JIJINI ARUSHA

KONDOM MPYA ZINAZOITWA ZANA ZAZINDULIWA JIJINI ARUSHA

 
Na Alice Mapunda,Arusha.
Muuguzi Mkuu  Mkoa wa Arusha,  Bi.Mwamini Juma Nyakwela, amezindua rasmi mpira wa kiume (Kondom),unaoitwa ZANA kwa mikoa ya Manyara na Arusha ambayo ipo katika kifungashio kipya,uzinduzi huo umefanyika katika kituo cha mafunzo ya afya(CEDHA) Jijini Arusha.

Uzinduzi huo umefanyika baada ya mipira hiyo kuwekwa katika vifungashio vipya na hivyo kubadili muonekano uliokuwa umezoeleka  zamani.

“Leo hii tunazindua mipira hii yakiume ambayo imebadilishwa kifungashio lakini ubora wake uko pale pale,watu endeleeni kuitumia,”amesema.

Watu wengi waliaacha kutumia mipira hii kwasababu haikuwa kwenye vifungashio vizuri na wakawa wanatumia aina nyingine ,lakini kwasababu Serikali inawajali wananchi wake ikaamua kubadili vifungashio ili wananchi waendelee kuzitumia zaidi.

Kutokana na tafiti mbalimbali zilizofanywa zilionyesha  asilimia 69 ya wanawake na asilimia 77 ya wanaume wanauelewa mzuri juu ya matumizi sahihi ya mipira ya kiume lakini ni asilimia 27 tu ndio wametumia mipira hii.

Aidha Kaimu Mkuu wa kitengo cha Elimu,Habari na Mawasiliano kwa mpango waTaifa wa kudhibiti UKIMWI kutoka Wizara ya fya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Bi. Edda Katikiro,amesema mipira hii ya jina la ZANA imeshasambazwa rasmi  kuanzia Juni 2016 na zilitengenezwa takribani  Milioni 21 lakini bado Wizara inaendelea kutengeneza nyingine zaidi.

Akisisitiza zaidi juu ya mipira hii yenye vifungashio vipya,amesema wananchi hawanabudi sasa watumie hii mipira kwasababu hakuna kilichobadilika zaidi ya kifungashio tu, na Serikali inatoa bure kwa nchi nzima.

“Hii ni ileile mipira ya kiume iliyokuwa inatumika tokea zamani mabadiliko haya ya vifungashio yasiwaogopeshe watu wakajua ni mipira mipya,”alisisitiza Edda.

Kutokana na dhana potofu iliyokuwepo katika jamii juu ya muonekana ambao haukuwa mzuri kwa hii mipira ya kiume hususani huko nyuma ikapalekea watu wengi kutoziamini kwa ubora wake na hata wengine kutozitumia kabisa.

Aidha amewata watu wajitaidi kupata elimu sahihi juu ya matumizi ya mipira hii, ilikupunguza au  ikiwezekana kutokomeza kabisa magongwa ya zinaa,UKIMWI na mimba zisizotarajiwa.

Kwa Mkoa wa Arusha maambukizi ya UKIMWI kwa mwaka 2016 ni asilimia 3.2 kulinganisha ni kiwango cha Taifa cha asilimia 5.1, hivyo kwa Mkoa kasi ya maambukizi ipo chini,na usambazaji wa mipira ya kiume tayari Mkoa ulishapeleka maombi yake nakupatiwa mipira hii aina ya ZANA na imeshasambazwa katika vituo vyote vya afya.

Uzinduzi kama huu umeshafanyika katika mikoa ya Mbeya na Mwanza na utaendelea zaidi kwa mikoa mingine na juhudi kubwa imeshawekwa kwa upande wa Serikali katika kuhakikisha mipira hii inatumika kwa kiasi kikubwa ili kufikia mwaka 2020 UKIMWI uwe umetokomezwa kabisa na wadau mbalimbali wazidi kushirikiana na Serikali katika mapambano hayo.
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa