Arusha
Home » » BRITAM YAADHIMISHA MIAKA 50 YA KUTOA BIMA

BRITAM YAADHIMISHA MIAKA 50 YA KUTOA BIMA


Katikati ni Mgeni rasmi mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini Mh.Mrisho Gambo ambaye alikuwa akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh.Daudi Ntibenda, akipongezana na Mkurugenzi wa Masoko BRITAM Kenya huku miale ya baruti ikihanikiza  ishara ya uzinduzi wa  shughuli zitakazokuwa zikifanywa na BRITAM katika jiji la Arusha wakati wa hafla hiyo katika hoteli ya Mount Meru

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini Mh.Mrisho Gambo akihutubia wageni katika hafla hiyo

Kulia ni Mgeni rasmi mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini Mh.Mrisho Gambo ambaye alikuwa akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh.Daudi Ntibenda, akifungua pazia ishara ya uzinduzi wa  shughuli zitakazokuwa zikifanywa na BRITAM katika jiji la Arusha wakati wa hafla hiyo katika hoteli ya Mount Meru
Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini Mh.Mrisho Gambo akipeana mikono na Mwenyekiti wa Bodi BRITAM Tanzania Bw.Michael Laizer ishara ya pongezi mara baada ya ufunguzi  


Mkurugenzi mtendaji BRITAM Tanzania Bw.Stephen Lokonyo akitoa historia ya utendaji wa  kampuni kuhusu kampuni yao wakati wa hafla hiyo katika hoteli ya Mount Meru (picha zote na  Dickson Mulashani)

 Mgeni rasmi mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini Mh.Mrisho Gambo ambaye alikuwa akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh.Daudi Ntibenda, akiefuatilia shughuli zilizokuwa zikiendelea wakati wa hafla hiyo katika hoteli ya Mount Meru
Kutoka kulia ni Afisa Mkuu wa Uendeshaji BRITAM Bw.Sodson Manatsa  akiwa na Meneja Masoko BRITAM Tanzania Bw.Godfrey Mzee wakifuatilia kwa makini hafla hiyo
Meza Kuu ambapo wageni rasmi waliketi katika hafla hiyo
Meneja BRITAM Tanzania tawi la Arusha Bi. Loisi Yatera akizungumza wakati wa ufunguzi wa hafla hiyo 
Kutoka kushoto ni Mbunge wa zamani wa jimbo la Arusha Mjini Mh.Felix Mrema, katikati ni Mkurugenzi wa Masoko BRITAM Kenya na mwisho ni Mkurugenzi BRITAM Kenya Bw.Stephen Wandera 
Meneja BRITAM Tanzania tawi la Arusha Bi. Loisi Yatera akiwatambulisha baadhi ya watendaji wa Kampuni hiyo mbele ya wageni waliohudhuria katika hafla hiyo
Sehemu ya wageni waliohudhuria hafla hiyo katika hoteli ya Mount Meru
Mbunge wa Arusha Mjini Mh.Godbless Lema pamoja na mke wake wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri katika hafla hiyo ndani ya Hoteli ya Mount Meru jijini Arusha
Mkurugenzi BRITAM Kenya Bw.Stephen Wandera akimsikiliza kwa makini mgeni rasmi wakati akihutubia wageni katika hafla hiyo
Habari na Woinde Shizza,Arusha.

Kampuni ya Bima ya Britam imeadhimisha miaka 50 ya kutoa huduma za bima nchini Tanzania huku ikiongoza katika utoaji wa huduma bora za bima za magari,nyumba ,mali pamoja na afya.

Sherehe za Maadhimisho hayo zimefanyika katika Hotel ya Mount Meru iliyoko jijini Arusha na kuudhuriwa na Viongozi wa kiserikali pamoja na Wadau wa Bima.

Afisa Mkuu wa  Kampuni hiyo  nchini Tanzania  Stephen Lokonyo amesema kuwa kampuni hiyo imejipanga vizuri kuwahudumia watanzania na kuwafikia watu wengi zaidi ili waweze kunufaika na huduma za bima .

Aliongeza kuwa wao kama kampuni ya bima ya Britam wamejipanga kuwasaidia wananchi mbalimbali wakiwemo wa juu pamoja na wachini kwakuanzisha bima za aina mbalimbali ikiwemo ya mali zao kama nyumba ,bima za afya pamoja bima ya kilimo kwa ajili ya wakulima pamoja na wafugaji.

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mrisho Gambo aliwataka mashirika ya bima kuwafikiria pia madereva bodaboda kwa kuwaanzishia bima za afya pamoja na bima za vyombo vyao ili pale wanapopata matatizo kama ya kuunguliwa na piki piki zao pamoja na kupata ajali waweze kusaidika kwa uraisi matibabu na kufidiwa pindi wanapopata ajali.

Alisema kuwa kumekuwa na pikipiki nyingi sana hivyo iwapo wataanzisha bima kwa ajili ya pikipiki wataweza kuwasaidia sana vijana pia wataweza kupata wateja wengi waotumia vyombo hivi.


Aidha mkuu huyo wa wilaya alihiasa  kampuni ya bima ya  Britam pamoja na kampuni zingine za bima kujikita  zaidi  kwa watu wenye kipato cha chini.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa