Home » » Walimu wastaafu wa sayansi kupewa ajira

Walimu wastaafu wa sayansi kupewa ajira

Philipo Mulugo
 
Serikali imetangaza neema kwa walimu wastaafu wa somo la sayansi kujitokeza na kupeleka majina yao Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ili waweze kupatiwa nafasi za kufundisha, kuziba pengo la ukosefu wa walimu hao nchini.
Hatua hiyo imechukuliwa ili kupunguza tatizo la upungufu wa walimu 26,000 uliopo hivi sasa hali inayoathiri zaidi wanafunzi wanaochukuwa masomo ya sayansi.

Hayo yalisemwa jijini Arusha na aliyekuwa Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo siku moja kabla ya kuvuliwa wadhifa huo, wakati akizungumza katika mahafali ya tano ya chuo cha ufundi Arusha (ATC) ambapo jumla ya wanafunzo 256 walitunukiwa vyeti vya astashahada, stashahada na shahada ya kozi mbalimbali.

Alisema endapo walimu hao wastaafu hawatajitokeza, serikali itaingia hasara kubwa kutokana na kuajiri walimu wa fani hiyo kutoka nje ya nchi. Mulugo alisema serikali itawaombea kibali wizarani walimu wastaafu wa masomo ya sayansi watakaojitokeza  ili waweze kufundisha katika shule mbalimbali kwa kipindi cha miaka miwili na watakaopenda kuendelea hata kwa miaka 10 watakubaliwa.

“Tumekuwa tukitangaza sana kujitokeza kwa walimu wastaafu wa masomo ya sayansi nchi nzima kuleta majina yao wizarani ili waweze kupata ajira kwani tuna upungufu mkubwa sana, na tangu tutoe matangazo hayo wamejitokeza walimu wastaafu 96 tu, na hao hawatoshi bado tunawakaribisha sana popote pale walipo,” alisisitiza Mulugo. 
SOURCE: NIPASHE

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa