Arusha
Home » » MKUU WA MKOA WA ARUSHA AWATAKA WATUMISHI WOTE WA HALMASHAURI YA NGORONGORO KUTIMIZA WAJIBU WAO

MKUU WA MKOA WA ARUSHA AWATAKA WATUMISHI WOTE WA HALMASHAURI YA NGORONGORO KUTIMIZA WAJIBU WAO




 Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh. Mrisho Gambo
 akiongea na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo,amewataka watumishi wote wa Mkoa wa Arusha kutekeleza 
wajibu wao kama watumishi na kuachana na 
mambo ya siasa ambayo yanarudisha 
maendeleo yawananchi nyuma.


Ameyasema hayo alipokuwa akiongea na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro alipofanya ziara ya siku moja Wilayani humo na kukutana na changamoto mbalimbali zikiwepo za migogoro ya ardhi.

Muheshiwa Gambo ameziagiza Halmashauri zote za Mkoa wa Arusha kuhakikisha inatatua migogoro yote ya ardhi na ile inayoshindikana kwa ngazi hiyo ndio ipelekwe kwenye ngazi ya Mkoa na yeye atakuwa tayari kuwasaidia.

Aidha ametaka kupewa ripoti ya fedha zinazotolewa na wafadhili katika kila Halmashauri napia zile zinazopelekwa kwa wafugaji zielezwe matumizi yake na yeye atapita kukagua hizo shughuli za maendeleo kwa wananchi ili ajiridhishe na matumizi yake kama ni halali au sio.

Alisema anataka kupata pia taarifa juu ya chakula kinachotolewa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa wananchi wa Wilaya hiyo kama kweli kinawafikia wahusika hususani wananchi wa hali ya chini.

"Ikibainika kuwa fedha za wafadhili na chakula cha msaada vyote vinatumika visivyo basi wahusika wajiandae kuwajibishwa ipasavyo, kwasababu tunatakiwa kuwatendea haki wananchi wetu na sivinginevyo",alisema Gambo.

Aidha aliwaomba wawekezaji wakishirikiana na madiwani waendelee kudumisha uhusiano mzuri baina ya wananchi na wawekezaji hao ili kwa pamoja maendeleo kwa wananchi yapatikane kwa wakati.

Muheshiwa Gambo alikuwa na ziara ya siku moja katika Wilaya ya Ngorongoro kwalengo lakufuatilia shughuli mbalimbali za maendeleo kwa wananchi.



0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa