Arusha
Home » » MKUU WA MKOA WA ARUSHA AWATAKA VIONGOZI WA WILAYAYA NGORONGORO KUCHAGUA ENEO LA FORODHA KATIKA MPAKA WA WILAYA HIYO NA KENYA

MKUU WA MKOA WA ARUSHA AWATAKA VIONGOZI WA WILAYAYA NGORONGORO KUCHAGUA ENEO LA FORODHA KATIKA MPAKA WA WILAYA HIYO NA KENYA

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo,awataka viongozi wa Wilaya ya Ngorongoro kuchagua eneo maalumu kwaajili ya ujenzi wa ofisi za forodha katika mpaka wa Ngorongoro na nchi ya Kenya. 

Ameyasema hayo alipo tembelea eneo la mpaka wa nchi ya Kenya na Tanzania kwa upande wa Wilaya ya Ngorongoro akiambatana na Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya mapato Tanzania(TRA) Bwana. Alphayo Kidata.  "Nawaagiza Viongozi wote wa Wilaya hii kuanzia Mkuu wa Wilaya,Mwenyekiti wa Halmashauri na diwani wa Kijiji cha Njoroi kukaa na wananchi nakisha kuamua ni eneo gani ambalo litafa kujenga ofisi zetu za forodha".



Alisema Serikali ya awamu ya tano ipo karibu sana na wananchi wa hali ya chini hususani katika kuwaletea maendelea hivyo wananchi wanatakiwa kushirikiana kikamilifu na Serikali yao. Amesema Serikali imeona kuna ulazima wakujenga ofisi za forodha katika Kijiji hicho ili kujipatia mapato kutoka kwa wageni wanaoingia na pia kupunguza uwingizaji wa mifugo kiholela.

 Ziara hiyo ya Mkuu wa Mkoa na Kamishina Mkuu wa TRA katika Wilaya ya Ngorongoro hususani katika Kijiji cha Njoroi ilikuwa na lengo  lakuona ni eneo gani litafaa kuwa na ofisi za forodha ambapo litapunguza uwingiaji wa wageni kutoka nchi jirani ya Kenya ambao wanaingia nchini Tanzania kwalengo lakujipatia mahitaji mbalimbali bila yakutozwa kodi.





0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa