Arusha
Home » » Wasanii wa wanofanya kazi ya u-dijey watakiwa kujisajili katika Chama kwa lengo kujenga misingi imara ya taalum hiyo.

Wasanii wa wanofanya kazi ya u-dijey watakiwa kujisajili katika Chama kwa lengo kujenga misingi imara ya taalum hiyo.



Naibu Waziri wa Habari Utamaduni , Sanaa na Michezo  akikabidhi vyeti vya usajili wa Chama cha Madijey nchini leo jijini Arusha kwa Mwenyekiti wa Chama hicho Bw.Yusuph Juma kuashiria uzinduzi wa chama hicho rasmi.

Na Anitha Jonas – MAELEZO

Arusha.
Wasanii wa wanofanya kazi ya u-dijey  watakiwa kujisajili katika Chama kwa lengo kujenga misingi imara ya taalum hiyo.
Hayo yamesemwa leo Jijini Arusha na Naibu Waziri wa Habari ,Utamaduni,Sanaa na Michezo alipozindua chama hicho rasmi katika mkutano wa wadau wa kisekta uliyofanyika  katika ofisi za Mkuu wa Mkoa ambapo alikutana na wadau mbalimbali.
“Kuanzishwa kwa chama hiki kuanashiria ni kwa kiasi gani wadau wa sekta ya sanaa wameelewa umuhimu wa kurasimisha kazi zao na hili litaongeza tija katika kujenga heshima ya kada hii ya madijey  katika nchi yetu kama ilivyokwa nchi zilizoendelea”,alisema Naibu Waziri Wambura.
Kwa upande wa Mwenyekiti wa Chama cha Madijey Bw.Yusuph Juma alisema wameamuo kuanzisha chama hicho cha madijey kwa kuwa sanaa hiyo imekuwa ikidharaulika kwa kiasi kikubwa imekuwa ikionekana kama siyo sekta rasmi bali ni uhuni .
“Usajili wa madijey katika chama utazingatia vigezo vya taalum pamoja na leseni za udijey   hii ni kwa lengo la kuimarisha sekta hii ili kuipa nguvu na kuifanya iheshimike kama kazi nyingine  za kisana na  sivinginevyo”,alisema Bw.Juma.
Pamoja na hayo Mwenyekiti huyo alisema madijey wengi nchini wamekuwa wakifanya kazi hiyo kwa kulipwa ujira mdogo ukilinganisha na masaa wanayokuwa  wakifanya kazi  hiyo,hivyo kwa kupitia umoja huo wataunda muongozo utakaosaidia kuboresha mazingira ya malipo yao.
Pia Bw.Juma ameiomba  serikali kusimamia suala la madijey wote nchini kujiunga katika chama hicho kwa lengo la kuunda umoja wao utakowasaidia kupata fursa mbalimbali za kimaendeleo ikiwemo kutafuta namna ya  kuongeza  maslai  yao.
Hata hivyo uongozi huo umetoa shukrani kwa Serikali kwa ushirikiano uliyowapa katika kupitisha chama hicho ambacho kimesajili katika Baraza la Sanaa la Taifa .
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa