Arusha
Home » » Serikali ya pongeza uongozi wa Trust St.Patrick Sport Academy

Serikali ya pongeza uongozi wa Trust St.Patrick Sport Academy



Anitha Jonas – MAELEZO

Arusha.
Serikali ya pongeza uongozi wa Trust St.Patrick Sport Academy  kwa uamuzi wa kujenga  Kituo cha Mafunzo ya Michezo chenye hadhi  ya Kimataifa.
Pongezi hizo zimetolewa leo jijini Arusha na Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni ,Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura alipotembelea eneo hilo litakalojengwa kituo hicho ambacho kitakuwa na Michezo ya aina mbalimbali pamoja na hoteli ya nyota tano.
“Serikali inaunga mkono jitihadi za ujenzi huu kwani kituo hichi kitakapo malizika tunaimani kitakuwa chachu  ya ukuaji wa vipaji vya michezo kwa watanzania na kutaongeza mafanikio ya sekta ya michezo na kuwezesha kupata ushindi katika michezo mbalimbali katika ngazi za Kimataifa,”alisema Naibu Waziri.
Naye Katibu Mkuu wa Kituo hicho Bi.Dinna Patrick  alimweleza Naibu waziri huyo chagamoto waliyonayo  katika eneo hilo la kuwepo kwa barabara inayogawa eneo hilo la kituo hicho ambalo ndiyo limekuwa kikwazo kinacho kwamisha ujenzi wa kituo hicho kuanza kwa haraka.
“Kituo hicho kitakuwa na uwanja wa mpira ambao utakuwa na uwezo wa kuchukua watu elfu ishirini ambao utakuwa wenye hadhi ya kimataifa na kituo hicho kinatarajiwa kuwa bora zaidi katika Kanda ya  Afrika Mashariki”,alisema Bi.Patrick.
Baada ya kupata malalamiko hayo Mheshimiwa huyo aliuagiza uongozi wa mkoa  kufuatilia suala hilo katika ofisi za Halimashauri na kusaidia suala hilo kupata ufumbuzi ili kuharakisha ujenzi wa eneo hilo kwani kumalizika kwake kutaleta faida kubwa  kwa wapenzi wa michezo.
Aidha ,Naibu waziri huyo alitoa wito kwa uongozi wa Trust St.Patrick Sports Academy kujenga pia chuo cha walimu wa michezo mbalimbali nchini kwani kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa walimu wa michezo na uhaba wa vyuo vya michezo nchini.
Hata hivyo watanzania wenye uwezo wametakiwa kujitokeza na kujenga vituo vya mafunzo ya michezo kwani michezo ni ajira na inaweza kuchangia pato kubwa katika nchi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa