Wafanyakazi wa kampuni ya Megatrade wakiwa katika picha ya pamoja na watoto wa kituo cha New Paradise kilichopo kata ya sokoni 1 jijini Arusha,wakionekana wenye furaha kabisa baada ya kukabidhiwa msaada huo wa vyakula mbalimbali kwa ajili ya kusherehekea sikuu ya krismasi na mwaka mpya .Meneja mauzo na masoko Goodluck Kway wa kampuni ya Megatrade Investment akiwa anamkabidhi mmoja wa watoto yatima katoni ya soda (mwenye T-shirt ya blue) ikiwa ni sehemu ya kuwapa matumaini mapya watoto hao waishio katika mazingira magumu,msaada huo wa vyakula mbalimbali umetolewa kwenye kituo hicho kwa ajili ya sikuu ya krismasi na mwaka mpya.Sehemu ya baadhi ya vitu vilivyotolewa na kampuni ya Megatrade Investment kupitia kinywaji chake cha K-vant Gin katika kituo cha watoto yatima cha New Paradise kilichopo kata ya sokoni 1 jijini Arusha kwa ajili ya kusherehekea Krisimasi na mwaka mpya.
Na Pamela Mollel,Arusha
KAMPUNI ya Megatrade Ivestment kupitia kinywaji chake cha K-vant Gin imetoa misaada ya vitu mbalimbali ikiwemo chakula kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu kwaajili ya sikukuu ya krismasi na mwaka mpya katika kituo cha New Paradise kilichopo kata ya sokoni 1 jijini Arusha
Akikabidhi msaada huo juzi kituoni hapo Meneja mauzo na masoko Goodluck Kway wa kampuni ya hiyo kupitia kinywaji chake cha K-vant Gin alisema utowaji wa misaada kwa makundi maalum yenye uhitaji ni utaratibu wao wa kurudisha faida waliopata kwa mwaka mzima kwa jamii
Alisema msaada huo walioutoa umegharimu kiasi cha shilingili Milioni moja, ambapo watoto hao watasherehekea sikukuu kama watoto wengine, huku akitoa rai kwa makampuni kujitokeza kuwasadia watu wenye uhitaji wa namna mbalimbali.
Misaada iliyokabidhiwa kituoni hapo ni pamoja na sukari,mafuta ya kula,mchele,katoni za soda,sabuni,kalamu,madaftari,unga wa ugali,unga wa ngano na maziwa.Mlezi mkuu wa kituo hicho Christopher Kaaya alisema kampuni hiyo imekuwa msaada mkubwa kwao na amewaomba waendelee na moyo huo wa kuwasaidia
“Mungu awazidishie sana kwa sababu wamekuwa watu wa karibu kwetu hata siku ya kwanza walituchangia katika ujenzi wa jengo hili na pia kila mwaka lazima watuletee zawadi za chrismasi na mwaka mpya”alisema Kaaya
Kituo hicho kinajumla ya watoto 24 wasichana wakiwa 14 na wavulana 10 ambapo idadi imeongezeka ukilinganisha na mwaka jana watoto walikuwa 20 tu kituoni hapo.
Chanzo;Michuzi blog
Chanzo;Michuzi blog
0 comments:
Post a Comment