Ngorongoro. Vijiji 17 vya Tarafa ya Ngorongoro
mkoani Arusha, vimepewa Sh 221 milioni, ili zitumike katika utekelezaji
wa miradi ya maendeleo katika mwaka wa fedha wa 2013/14.
Fedha hizo zimetolewa na Baraza la Wafugaji wa tarafa hiyo.
Ofisa mtendaji wa baraza hiyo, Parkepo Nakoroi, alisema kila kijiji kitapata Sh 13 milioni.
Alisema fedha hizo, zimetolewa baada ya baraza kupokea mgao wa Sh2 bilioni kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment