Arusha
Home » » UTALII WA NDANI WAZIDI KUPATA MASHIKO ,WASOMI CHUO KIKUU SMMUCo WATEMBELEA HIFADHI YA NGORO NGORO

UTALII WA NDANI WAZIDI KUPATA MASHIKO ,WASOMI CHUO KIKUU SMMUCo WATEMBELEA HIFADHI YA NGORO NGORO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Simba dume  akiwa anaunguruma 
Simba jike akiwa amepumzika kwenye nyasi 
Na Dickson Mulashani

Suala la utalii wa ndani limeonekana kupata mashiko baada ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Stefano Moshi Memorial University College (SMMUCo) kuhamsika na kuamua kutembelea hifadhi ya taifa ya Ngoro ngoro ili kujionea vivutio vya kipekee vinavyopatikana humo.
Wanafunzi hao wakiwa katika geti la kuingia hifadhi ya Ngoro ngoro

Akizungumzia safari hiyo mmoja wa wanafunzi hao Emmanuel Kalenzi amesema waliguswa kupanga ziara hiyo kuunga mkono wadau mbali mbali wanaohamasisha utalii wa ndani ili kuweza kuwa mabalozi kwa wengine. “Sisi kama wasomi ndio tunapaswa kuwa mabalozi kwa jamii inayotuzunguka na ili uwe balozi mzuri basi uwe umashajionea kwa macho”  alisema.

Nyati dume mwenye umri mkubwa ambaye tayari ametengwa na kundi lake 

Ndege aina ya Cranes nao wanapatikana katika eneo la crater

Nyumbu akiwa amepumzika mara baada ya kula nyasi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa