Arusha
Home » » Balozi wa Norway nchini awatunuku wahitimu Chuo cha Ufundi Arusha

Balozi wa Norway nchini awatunuku wahitimu Chuo cha Ufundi Arusha

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Balozi wa Norway nchini Tanzania,Hanne -Marie Kaarstad ambaye alikua mgeni rasmi katika Mahafali ya Saba ya Chuo cha Ufundi Arusha (ATC) akiwatunuku Vyeti, Stashahada na Shahada wahitimu katika fani za Uandisi Umwagiliaji,Umeme,Ujenzi,Mawasiliano Anga ,Mitambo na Kompyuta Januari 16,2016.
Baadhi ya wahitimu wa fani ya Uandisi Mitambo wakifurahia mara baada ya kutunukiwa Stashahada zao.
Wahitimu wakifatilia kwa makini hotuba mbalimbali.
Balozi wa Norway nchini Tanzania,Hanne -Marie Kaarstad ambaye alikua mgeni rasmi katika Mahafali ya Saba ya Chuo chaUfundi Arusha (ATC) akiwa katika picha ya pamoja na wanachuo wanaobaki.
Balozi wa Norway nchini Tanzania, Hanne -Marie Kaarstad (kulia)akipokea zawadi kutoka idara ya Uandisi Madini.
Balozi  Hanne -Marie Kaarstad akifurahia kazi za wanachuo alipotembelea maonesho yaliyoandaliwa kwaajili yake.
Wanachuo wanaobaki walionegesha mahafari hayo kwa bendera za kuvutia.
Balozi Hanne -Marie Kaarstad  na Mkuu wa Chuo hicho, Dk Richard Massika aliyevaa tai nyekundu wakipata maelezo kwenye idara ya Umwagiliaji.
Furaha ya kuhitimu ilitawala.
Mkuu wa Chuo cha Ufundi Arushab (ATC) Dk Richard Massika (kulia) akifafanua jambo kwa mgeni rasmi.
Balozi wa Norway, Hanne -Marie Kaarstad (wa pili kushoto mbele) akiwa na wageni mbalimbali na Wakuu wa Idara mbalimbali za Chuo katika picha ya pamoja.
Burudani kwa wahitimu ilikuwepo kunogesha mahafali hayo. Imeandaliwa na www.rweyemamuinfo.blogspot.com – 0713 821586, Arusha.


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa