Arusha
Home » » PINDA APONGEZA SEKTA YA UTALII ARUSHA

PINDA APONGEZA SEKTA YA UTALII ARUSHA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda ameimwagia sifa hoteli maarufu ya Ngurdoto yenye hadhi ya nyota tano, iliyopo nje kidogo ya jiji la Arusha, kutokana na kuwa na ukumbi mkubwa wa kisasa wenye uwezo wa kuketisha watu zaidi ya 3,000 kwa wakati mmoja na kueleza kuwa ukumbi huo ni mkombozi kwa sekta ya utalii nchini.

Aidha alikitaka kituo cha kimataifa cha mikutano cha Arusha, AICC kuboresha kumbi zake ili ziendane na wakati huku akitahadharisha kwamba upo uwezekano wa kituo hicho kukosa mikutano iwapo kitashindwa kuboresha kumbi zake ziwe na hadhi ya kimataifa.

Kauli hiyo ameitoa jijini hapa wakati akifungua mkutano wa wadau wa maji unaofanyika katika ukumbi huo huku akitumia muda mwingi kutazama mandhari ya ukumbi huo.

"Kwa kweli hili jengo ni la kisasa sana nimetembea sehemu nyingi hapa nchini sijawahi kuona ukumbi wa kisasa kama huu, kwa kweli Mrema (mmiliki wa hoteli) ametuokoa sana, hii ni changamoto kwa AICC wajitahidi kuboresha kumbi zao vinginevyo watapigwa mweleka,"alisema Bw.Pinda.

Pinda aliongeza kuwa Tanzania kuwa na ukumbi wa kisasa kama huo ni heshima kwa taifa na hivyo serikali itajitahidi kuleta mikutano ya kutosha.

Awali mkuu wa mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, alimweleza Waziri Mkuu Pinda kwa kuitaka serikali iangalie uwezekano wa kuhamishia mikutano mingi mbalimbali ya kitaifa na kimataifa kufanyika jijini hapa kwa kuwa tayari inao vigezo vyote vya kufanikisha mikutano hiyo.

Bw.Mulongo alisema ni bora mikoa mingine ikakubali kuuachia mkoa wa Arusha kuandaa mikutano mbalimbali kutokana na vigezo vilivyopo zikiwemo hoteli nyingi zenye kumbi za kisasa, huku akitolea mfano ukumbi huo wa Ngurdoto maarufu kwa jina la Tanzania Convention Center.

"Karibuni sana Arusha yale mambo yetu ya zamani tumeshaacha na wale wanaoamini wangekutana na mabomu sasa hayapo tena, karibuni kwenye ukumbi mpya wa kisasa zaidi, mheshimiwa waziri mkuu lazima mikoa mingine wakubali kuuachia mkoa wa Arusha kuandaa mikutano mbalimbali kwa sababu vigezo vyote tunavyo,"alisema Bw.Mulongo.

Aidha alisema mkoa wa Arusha ni kituo cha utalii na vivutio vingi vya kumfanya mgeni afurahie mandhari yaliyopo hivyo aliongeza kwa kuwataka wadau mbalimbali kuwa hakuna haja ya kupeleke mikutano sehemu nyingine

Chanzo:Majira

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa