Arusha

JENGO LA MAMLAKA YA HIFADHI YA NGORONGORO KUWA KIVUTIO CHA KIHISTORIA CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA UTALII JIJINI ARUSHA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.


Na Hamza Temba - WMU
........................................................
JENGO la kitega uchumi la Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro jijini Arusha ambalo ujenzi wake unatarajiwa kukamilika mwezi juni mwaka huu litakuwa kivutio cha kihistoria cha utoaji wa huduma za utalii hapa nchini.

Hayo yameelezwa jana na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla muda mfupi baada ya kukagua jengo hilo ambalo linasemekana kuwa refu kuliko majengo yote jijini Arusha likiwa na jumla ya ghorofa 18.

Alisema jengo hilo ambalo linatizamana na Round About ya AICC katikati ya jiji hilo, limekusudiwa kuwa Kituo Kimoja (One Stop Centre) cha shughuli zote za utoaji wa huduma za utalii jijini humo kuanzia uwekezaji, utangazaji na menejimenti kwa ujumla.

Alisema jengo hilo litatoa fursa kwa wadau mbalimbali wanaotoa huduma za utalii kuweka ofisi zao ikiwemo mabenki, watoa huduma za usafiri, mashirika ya ndege, mawakala wa safari za utalii na huduma, maduka ya bidhaa za utalii na mahoteli.

"Tutapamba pia jengo hili na" live screen" (Mabango ya Video Mubashara) za vivutio, hivyo wanyama wakiwa wanapita huko porini watakuwa wanaonekana "LIVE" (Mubashara) kwenye jengo hili kupitia LED Screen ambazo zitakuwa zimezunguka jengo hili" alisema Dk. Kigwangalla.

Alisema huduma nyingine zitakazotolewa katika Jengo hilo ni pamoja na zile za kuangalia jiji la Arusha kupitia darubini, huduma za burudani ikiwemo kumbi za starehe na migahawa.

Kwa upande wake Mkandarasi wa jengo hilo, Mhandisi Bismas Meela wa Kampuni ya Inter-Consult limited alisema ujenzi wa jengo hilo ambalo ulianza mwezi Novemba, 2013 unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi juni mwaka huu.

Alisema jengo hilo ambalo lina uwezo wa kupaki magari 67 kwa wakati mmoja katika ghorofa za chini linagharimu shilingi za Kitanzania bilioni 45.

Katika ziara hiyo ya siku moja ya ukaguzi wa jengo hilo, Dk. Kigwangalla aliongozwa na Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Dk. Fredy Manongi na Naibu Mhifadhi wa Huduma za Uendeshaji wa Mamlaka hiyo, Asangye Bangu. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa pili kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Naibu Mhifadhi wa Huduma za Uendeshaji wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Asangye Bangu kuhusu jengo la kitega uchumi la mamlaka hiyo lililopo katikati ya Jiji la Arusha ambalo limekusudiwa kuwa Kituo Kimoja cha shughuli zote za utoaji wa huduma za utalii jijini humo kuanzia uwekezaji, utangazaji na menejimenti kwa ujumla. Kulia ni Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka hiyo, Dk. Fredy Manongi.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiangalia mandhari ya Jiji la Arusha akiwa juu ya Jengo la kitega uchumi la Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro. Kutoka kulia ni Naibu Mhifadhi wa Huduma za Uendeshaji wa Mamlaka hiyo, Asangye Bangu na  Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka hiyo, Dk. Fredy Manongi. 
Dk. Kigwangalla akiendelea kupata maelezo kuhusu jengo hilo kutoka kwa Naibu Mhifadhi wa Huduma za Uendeshaji wa mamlaka hiyo, Asangye Bangu. 

 Dk. Kigwangalla na msafara wake wakiangalia umbo la uso wa simba uliotengengenezwa katika moja lango la kuingilia kwenye lift ndani ya jengo hilo. Milango yote ya kuingilia kwenye lift ndani ya jengo hilo itapambwa kwa taswira mbalimbali za wanyamapori.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akishuka kwenye ngazi maalum zinazotumia nishati ya umeme ndani ya Jengo hilo. Kulia ni Naibu Mhifadhi wa Huduma za Uendeshaji wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Asangye Bangu na nyuma yake ni Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka hiyo, Dk. Fredy Manongi. \
Waziri Kigwangalla akikagua kabati la kuhifadhia vitu katika moja ya Hotel Aprtment ndani ya jengo hilo. Kulia ni Naibu Mhifadhi wa Huduma za Uendeshaji wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Asangye Bangu.
Muonekano wa jengo hilo kutokea barabara ya Makongoro Jijini Arusha.

MKURUGENZI MKUU NIDA ATEMBELEA NA KUKAGUA HATUA ZA UJENZI WA OFISI ZA WILAYA MKOANI ARUSHA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA Ndg. Andrew W. Massawe akiweka saini kwenye kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Wilaya ya Longido na kupokelewa na Katibu Tawala.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA (kushoto), akifuatiwa na Afisa Usajili Wilaya ya Longido Ndg. Tarimo wakisikiliza taarifa ya mwenendo wa Usajili wananchi kwa Wilaya ya Longodo iliyowasilishwa na Katibu Tawala Ndg. Toba Nguvila (Katikati). K kulia ni Ndugu Alphonce Malibiche Kaimu Mkurugenzi Idara ya Uzalishaji.
  Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA Ndg. Andrew W. Massawe (wa kwanza kushoto) akiwa ameambatana na Katibu Tawala Wilaya ya Longido Ndg.Toba Nguvila wakiwa wamewasili kukagua ujenzi wa jengo la Ofisi za NIDA wilaya ya Longido na kupokelewa na mkandarasi wa ujenzi ndugu Kim na maafisa wengine.
  Muonekano wa Ofisi ya Usajili Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Wilaya ya Longido mkoani Arusha, ikiwa katika hatua za mwisho za ujenzi.



Kaimu Mkurugenzi Mkuu (NIDA) Ndg. Andrew W. Massawe ametembelea na kukagua hatua za ujenzi wa majengo ya ofisi katika Mkoa wa Arusha; na kukutana na viongozi mbalimbali wa mkoa huo kujadili maendeleo ya zoezi la Usajili wananchi linaloendelea nchini kote.

Ujenzi wa Ofisi za NIDA unaoendelea katika Wilaya za Arusha, Arumeru na Longido ni mradi wa mkopo wenye masharti nafuu unaofadhiliwa na Serikali ya Korea Kusini.

Akizungumza na Katibu Tawala Wilaya ya Longido mara baada ya kukamilisha ukaguzi wa majengo hayo; ndugu Massawe amesema majengo hayo yatawezesha NIDA kufanikisha malengo ya Usajili kwa asilimia kubwa, pamoja na kurahisisha usafirishaji wa Data kwenda makao makuu ya uzalishaji Vitambulisho kwakuwa majengo hayo yamejengwa kisasa na yana miundombinu ya kuwezesha uzalishaji wenye kukidhi vigezo vinavyohitajika kutokana na teknolojia inayotumika.

Wilaya ya Longido Mkurugenzi huyo alipokelewa na Katibu Tawala Ndg. Toba Nguvila kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo ambaye ameishukuru NIDA kwa hatua kubwa ya ujenzi wa jengo la kisasa kwenye wilaya mpya ya Longido; ambalo si tu litasaidia kuondosha uhaba wa Ofisi lakini kuwezesha Taasisi nyingine kama RITA na Uhamiaji kupata ofisi zitakazowahudumia wananchi kwa ufanisi mkubwa zaidi tofauti na hali ya sasa.

Kwa mujibu wa Mkandarasi Kampuni ya KT –Korea; Ujenzi wa majengo hayo unatazamiwa kumalizika mapema mwezi Mei mwaka huu; na kukabidhiwa NIDA kwa ajili ya kuanza matumizi.


 

WATUMISHI WATANO NCAA WAPANDISHWA KIZIMBANI KWA KUISABABISHIA SERIKALI HASARA YA DOLA ZA KIMAREKANI 35,500

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Na.Vero Ignatus Arusha.

Wafanyakazi watano wa Mamlaka ya Hifadhi ya
Ngorongoro(NCAA])wamefikishwa mahakamani leo kwa kosa la kuisababishia hasara serikali na kusababisha hasara ya dola za Kimarekani 35,500.

Watuhumiwa waliofikishwa kizimbani na kukabilia na shitaka moja ni pamoja na Joseph Mtwala{36},John Mlambo{42},Mwahu Yunus {38},Mery Njau{38} na Catherini Edward {33}.

Watuhumiwa hao wote kwa pamoja walisomewa shitaka moja na Mwendesha Mashitaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa{TAKUKURU} ,Adamu Kilongozi akiwa na Hamidu Simbano na Richard Jacopiyo kuwa walitenda kosa hilo kati ya desemba 25 mwaka 2013 na juni 6 mwaka 2014.

Kilongozi alidai mahakamani hapo kuwa watuhumiwa hao wakiwa katika lango la Nabi Mkoani Mara na lango kuu la Loduare Mkoani Arusha watuhumiwa hao walisababishia serikali hasara ya fedha za Kimarekani kiasi hicho wakiwa watumishi wa NCAA.

Mwendesha mashitaka huyo alisoma shitaka hilo mbele ya Hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha,Bernad Nganga na kueleza kuwa walifanya kosa hilo huku wakijua ni kinyume na sheria.


Watuhumiwa wote walikana shitaka hilo na walipewa dhamana ya fedha taslimu shilingi milioni 7.9 au mali isiyohamishika yenye thamani hiyo na taratibu za dhamana zilikuwa zikiendelea .

Mwendesha mashitaka wa TAKUKURU alisema kuwa ushahidi wa kesi hiyo umekamilika na aliiomba mahakama hiyo kupanga Tarehe ya kuanza usikilzwaji wa awali
Watuhumiwa wote watano wamepelekwa rumande kwakushindwa kukidhi masharti ya dhamani ,ambapo watasomewa hoja za  awali April 10 mwaka huu.




JAFO AGIZA MAAFISA HABARI SERIKALINI KUINGIA KWENYE VIKAO VYA MAAMUZI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais ,Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo akizungumza wakati wa kufunga Kikao kazi cha 14 cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini kilichofanika kwa siku tano katika Ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa (AICC) jijini Arusha.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Sanaa ,Utamaduni na Michezo ,Susan Mlawi akizungumza wakati wa ufungaji wa Kikao Kazi cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikali kilichofanyika jijini Arusha.
Waziri Jafo akiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari ,Maelezo ,Dkt Hassan Abbas pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini (TAGCO) Pascal Shelutete wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu Wizara ya Habari ,Sanaa,Utamaduni na Michezo ,Susan Mlawa (hayupo pichani) .
Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini (TAGCO) Pascal Shelutete akizungumza wakati wa kuhitimisha siku tano za Kikao kazi cha maafisa hao kilichofanyika jijini Arusha.
Waziri wa Nchi ,Ofisi ya Rais ,Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo akikabodhi cheti kwa Mwenyekiti Mstaafu wa TAGCO ,Innocent Mungi ikiwa ni ishara ya utambuzi wa mchango wake katika chama hicho. 
Waziri wa Nchi ,Ofisi ya Rais ,Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo akikabodhi cheti kwa Mmoja wa viongozi wa zamani wa TAGCO,Silvia Lupembe ambaye pia ni Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa Chuo Kikuu cha Mzumbe ,Morogoroikiwa ni ishara ya utambuzi wa mchango wake katika chama hicho. 
Waziri wa Nchi ,Ofisi ya Rais ,Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo akikabodhi cheti Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika la Ugavi wa Umeme (TANESCO) Leila Muhaji kutambua mchango wa Shirika hilo katika kufanikisha kikao kazi cha maafisa Habari ,Mawasiliano na Uhusiano  Serikalini kilichofanyika jijini Arusha. 
Mgeni rasmi katika ufugaji wa Kikao kazi cha 14 cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini ,Waziri wa Nchi ,Ofisi ya Rais,Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemeni Jafo akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa kikao hicho.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

SERIKALI imeziagiza Halmashauri kuhakikisha Maafisa Habari wanaingia katika vikao vya maamuzi ili waweze kupata na kutoa habari sahihi huku akiwatuhumu baadhi ya maafisa wa Halmashauri kuwa huendi ndio wanazuia maafisa habari kuingia katika vikao kwa lengo la kuficha baadhi ya taarifa.

 Agizo hilo la serikali limetolewa na Waziri wa nchi ofisi ya Rais ,Serikaliza Mitaa(TAMISEMI) Seleman Jafo wakati wa kufunga kikao kazi cha 14 cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini kilichofanyika jijini Arusha kwa muda wa siku tano.

 afo pia ameziagiza Halmashauri kutenga fungu katika Bajeti zao kwa ajili ya ununuzi wa vifaa kwa ajili ya Maafisa Habari ili kusaidia katika kutekeleza majukumu yao kwa urahisi ya kuhabarisha umma shughuli mbalimbali za maendeleo zinazofanywa Serikali.

 Mapema katika hotuba yake Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Sanaa,Utamaduni na Michezo ,Susan Mlawi amesema kikao kazi hicho kimekuwa na manufaa makubwa kwa Maafisa HABAI hao na kwamba kwa sasa watakuwa na uwezo mkubwa wa kuisemea serikali.

 Kikao hicho kimemalizika kwa Mgeni rasmi Waziri ofisi ya Rais ,Serikali za mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo kutunuku vyeti kwa Wadhamini wakuu waliofanikisha mkutano huo pamoja na viongozi wa zamani wa Chama cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini (TAGCO).

 Mwisho  

DR. HASSAN ABASS AZINDUA TOVUTI YA MISA TANZANIA, JIJINI ARUSHA


 Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt.Hassan Abbas(wa kwanza Kulia) na  Mwenyekiti wa MISA Tanzania Bi. Salome Kitomari(wa kwanza kushoto) wakizindua rasmi Tovuti ya MISA Tanzania inayopatikana hapa www.tanzania.misa.org
 Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt.Hassan Abbas(wa kwanza Kulia) na  Mwenyekiti wa MISA Tanzania Bi. Salome Kitomari(wa kwanza kushoto)pamoja na wadau mbalimbali ambao hawapo pichani wakipata maelezo kuhusiana na Tovuti ya MISA Tanzania kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa MISA Tanzania Bw. Gasirigwa
Sengiyumva ambaye hayupo pichani.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa MISA Tanzania Bw. Gasirigwa Sengiyumva(kulia) kulia akiendelea kutoa maelezo mbali mbali na vitu ambavyo vinapatikana katika Tovuti ya MISA Tanzania 
 Picha ya pamoja baada ya uzinduzi wa Tovuti ya MISA Tanzania Jijini Arusha.

DKT.ABBAS APONGEZA UTAFITI ULIOFANYWA NA MISA TANZANIA KWA KUSHIRIKIANA NA CPESA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt.Hassan Abbas,akizungumza na Maafisa Habari, Asasi za Kiraia pamoja na  waandishi wa habari  wakati kupokea taarifa ya   mrejesho wa utafiti uloiofanywa na MISA Tanzania kwa kushirikiana na CIPESA


Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa MISA Tanzania Bw.  Gasirigwa Sengiyumva akiuliza maswali wakati wa mapitio ya ripoti ya upatikanaji wa Taarifa Tanzania uliofanywa na Taasisi ya vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika(MISATAN) ikishirikiana na Taasisi ya CIPESA ya nchini Uganda.


Wakili wa Mahakama Kuu Tanzania Bw. James Marenga akitoa mrejesho wa utafiti uloiofanywa na MISA Tanzania kwa kushirikiana na CIPESA kwa Maafisa Habari wa Serikali, Asasi za Kiraia pamoja na Waandishi wa Habari Jijini Arusha.
Bi. Ashnah Kalemera kutoka CIPESA akiwasilisha mambo mbalimbali yanayohusiana na upatikanaji wa Taarifa katika ukanda wa Afrika Mashariki


Bi. Juliet Nanfuka kutoka CIPESA akizungumza jambo wakati wa kupokea taarifa ya utafiti iliyofanywa na MISA Tanzania kwa kushirikiana na CIPESA


Baadhi ya wadau mbàlimbali pamoja na waandishi  katika mkutano huo


Mwandishi wa Gazeti la Habari leo Veronica Mheta akichangia mada katika mkutano huo


Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO)  Bw. Paschal Shelutete akijibu maswali mbalimbali wakati wa  mapitio ya ripoti ya upatikanaji wa Taarifa Tanzania uliofanywa na Taasisi ya vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika(MISATAN) ikishirikiana na Taasisi ya CIPESA ya nchini Uganda


Kaimu mkurugenzi wa MISATAN nchini Gasirigwa Sengiyumva (wa kwanza kushoto)akiwa na mmiliki wa Wazalendo Blog,Gadiola Emmanuel (mwenye skafu nyekundu shingoni) wakati wa kusikiliza wadau wanatarajia nini baada ya kusikiliza ripoti ya utafiti.
Mwenyekiti wa MISA Tanzania Bi. Salome Kitomari akitoa neno la Shukurani ikiwa ni pamoja na kumshukuru Msemaji Mkuu wa Serikali Hassan Abbas kwa ushiriki wake,Maafisa habari mbalimbali wa Serikali, Wadau kutoka Asasi za Kiraia pamoja na waandishi wa Habari.



 Mafunzo yakiendelea katika Hotel ya Impala Jijini Arusha.




Na.Vero Ignatus Arusha.



MSEMAJI Mkuu wa Serikali Dkt.Hassan Abbas amesema Maafisa Mawasiliano serikalini bado wanakabiliwa na changamoto kutoka kwa mabosi wao, ikiwano wengine kutokutaka habari zao zisikike kwenye vyombo vya habari.



Dkt.Abbas aliyasema hayo jana mjini hapa wakati mapitio ya ripoti ya upatikanaji wa Taarifa Tanzania uliofanywa na Taasisi ya vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika(MISATAN) ikishirikiana na Taasisi ya CIPESA ya nchini Uganda.



Alisema kupitia ripoti hiyo aliyoiunga mkono na kuisoma vyema atahakikisha maofisa mawasiliano zaidi ya 300 wanaokutana mjini Arusha wanapata utafiti huo."Nimesoma utafiti huu, kurasa zote upo vizuri, niwaombe muendelee kufanya tafiti kama hizi kwani ni chakula kwetu," alisema Dkt. Abbas.



Akizungumzia utafiti uliofanywa katika mikoa 7 na MISATAN Wakili wa mahakama kuu James Marenga amesema ofisi za halmashauri ya mikoa ya Arusha na kigoma ,walau ndiyo zimeonekana ndiyo wanafanaya vizuri katika kuwa wazi katika utoaji wa taarifa kuliko ofisi za mikoa.



Dodoma manispaa,halmashauri ya Jiji la mbeya,Kigoma ofisi ya mkuu Arusha, ofisi ya mkuu wa mkoa Mwanza hakukuwa na ushirikiano,vilevile mkoa wa Mtwara hakukuwa na ushirikiano ,Dar ni katika halmashari ya Jiji,Kwahiyo Utafiti huo ulikuwa umegawanya utoaji  wa taarifa kwa ofisi za mkuu wa mikoa na ofisi za halmashauri au za Majiji katika mikoa iliyochaguliwa.



Moja ya mapendekezo yaliyotolewa baada ya utafiti huo vitengo vya watoa taarifa vinaimarishwa kama inavyotakiwa  katika sheria ya haki  kupata taarifa ya mwaka 2016.Vilevile utafiti huo unasisitiza kuwepo na uwazi katika utoaji wa taarifa haswa kwenye taasisi za serikali.
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa