Mwandishi wetu, Monduli 

 

Taasisi ya wanahabari ya usaidizi wa Jamii za Pembezoni (MAIPAC) imezindua mradi wa

 uhifadhi wa mazingira kwa kutumia maarifa ya asili huko Halmashauri 

ya Monduli aliahidi kutoa kiwanja kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha kujifunza maarifa ya asili.

 

Mradi huo wa Mazingira unafadhiliwa na Mfuko wa Mazingira Duniani(GEF) 

kupitia program ya miradi midogo ambayo inasimamiwa na Shirika la

 Maendeleo la Umoja wa Mataifa(UNDP) na kuratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira).

 

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Monduli mkoa wa Arusha,Isack 

Joseph amezindua mradi huo leo, Julai 6,2024,katika hafla

 iliyofanyika hoteli ya Makambo te makuti iliyopo Kigongoni mto wa mbu wilaya ya Monduli.

 

Joseph akizungumza katika uzinduzi huo , alipongeza

 taasisi ya wanahabari wa MAIPAC kwa kubuni mradi huo. 

\ambao unasaidia vita dhidi ya athari za mabadiliko ya Tabia nchi.