Arusha
Home » » HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA YASAINI MKATABA WA MAKUBALIANO YA URAFIKI NA MANISPAA YA HUANGSHI – CHINA

HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA YASAINI MKATABA WA MAKUBALIANO YA URAFIKI NA MANISPAA YA HUANGSHI – CHINA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.




Halmashauri ya Jiji la Arusha mapema leo hii imesaini mkataba na kufanya makabidhiano   ya Mkataba wa Makubalino (MOU)   na baadhi viongozi wa Manispaa ya Huangshi – China waliotembelea Jiji hili kwa lengo hilo.
Makubaliano hayo ya  Mjidada (Sistership) unalenga kuimarisha urafiki baina ya Halmashauri ya Jiji la Arusha na Manispaa ya Huangshi,  kubadilishana mbinu za kiutawala  na kushirikiana katika nyanja mbalimbali ikiwemo biashara na uchumi, Sayansi na Teknolojia pamoja na Elimu na utamaduni.
Akizungumza katika Hafla hiyo ya Utiaji Saini Mstahiki Meya wa Jiji  Mh. Kalisti Lazaro amesema huu ni mwanzo mzuri kwa Jiji la Arusha kujitangaza  katika Miji Mikubwa Duniani inayoweza kutoa  fursa kwa jamii ya watu wa Arusha.
Naye Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Ndg. Athuman Kihamia alisisitiza kuwa Uhusiano huu utasaidia kuimarisha mifumo ya kiutendaji katika maeneo yale ambayo Mji wa Huangshi wamefanikiwa na hii itasaidia katika kutoa huduma bora kwa wananchi.
Kiongozi wa Msafara kutoka Huangshi ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Jumuiya wa watu wa Huangshi Bw. Wang Bin amesema Arusha ni Mji wa kwanza Afrika kuingia nayo makubaliano ya kuanzisha Mji Dada na hii ni kwa sababu ya mazingira rafiki ya uwekezaji yanayopatikana katika Jiji hili na zaidi ukuaji wa Mji unaohamasisha biashara kufanyika wakati wote.
Halmashauri ya Jiji ina mahusiano na miji kumi na mbili Duniani na kati ya hiyo Miji Minne iko katika Jamhuri ya watu wa China.



















 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa