Arusha
Home » , , » MEYA WA JIJI LA ARUSHA AWATUNUKU VYETI WANAHABARI (AJTC)

MEYA WA JIJI LA ARUSHA AWATUNUKU VYETI WANAHABARI (AJTC)


 Meya wa Jiji la Arusha Kalisti Lazaro akikabidhiwa Zawadi na Mkurugenzi wa Mafunzo wa Chuo cha Arusha Journalism Training College (AJTC)  Joseph Mayagila katika Mahafali ya chuo hicho yaliyofanyika chuoni hapo
 Wahitimu wa Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji  Arusha (AJTC) wakirusha kofia juu ishara ya kuonyesha kutunukiwa vyeti vya Shahada na Stashahada.
 picha ya pamoja na wahitimu
Meya wa Jiji la Arusha Kalisti Lazaro akimtunuku cheti cha stashahada ya Uandishi wa Habari na Utangazaji  Editha Makundi wa Chuo cha Arusha Journalism Training College (AJTC),wawatu kulia ni Mkurugenzi wa Mafunzo wa Chuo cha Arusha Journalism Training College (AJTC)  Joseph Mayagila.
Meya wa jiji la Arusha Kalisti Lazaro akizungumza katika Mahafali ya Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji  Arusha (AJTC) ,Kulia ni Mkurugenzi wa Mafunzo katika Chuo hicho Joseph Mayagila,kushoto ni Diwani wa kata ya Themi ,Melans Kinabo.Picha na Ferdinand Shayo











Meya wa Jiji la Arusha Kalisti Lazaro amewatunuku zaidi ya wahitimu 50 waliohitimu katika Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji  (AJTC) huku akiwataka kuwa mstari wa mbele katika kupigania haki za jamii na kuleta mabadiliko kupitia kalamu zao.



Kalisti amewataka Wanahabari kujikita katika kuandika habari za kijamii zitakazosaidia kutatua changamoto zinazoikabili jamii na kuleta suluhu kwenye matatizo ya jamii.



Ameishauri serikali kuangalia upya mswada wa habari na kuufanyia marekebisho katika vipengele ambavyo vinaminya haki ya habari.



Mkurugenzi wa Mafunzo katika Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji ,Joseph Mayagila amesema kuwa tasnia ya habari ni tasnia muhimu katika kuchochea maendeleo ya nchi kwani bila taarifa hakuna maendeleo.



Alisema kuwa ni vyema serikali ikatazama upya utekelezaji wa sheria mpya na kufanyia kazi mapungufu ili wanahabari waendelee kuwahabarisha Watanzania.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa