Home » » BODABODA WATAKA KUTOFAUTISHWA NA WAHUNI.

BODABODA WATAKA KUTOFAUTISHWA NA WAHUNI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
CHAMA cha waendesha bodaboda Arusha (Uwapa), kimeiomba serikali kuweka alama maalumu itakayowatofautisha wao na waendesha pikipiki binafsi kudhibiti wahuni wanaotumia jina lao kufanya maandamano na matukio maovu.
Kimeyasema hayo kutokana na maandamano yaliyofanyika mapema wiki hii na kudai hakiwatambui waliofanya maandamano hayo, chama hicho hakina taarifa kuhusu maandamano hayo. Mwenyekiti wa Uwapa, Godlight Rugemalila, alisema ametoa taarifa polisi kutokana na maandamano hayo kulaani kitendo hicho si sahihi.
Aliwataka waendesha bodaboda wote ikiwa wana jambo linalowakabili, kwa kuwa uongozi upo, wafuate utaratibu badala ya kukurupuka. Rugemalila alisema kuwepo kwa waendesha pikipiki waliosajiliwa na Uwapa ambao pia wanakabiliwa na tatizo la kutokuwa na vituo maalum na wengine wa kawaida ambao nao hujiingiza katika biashara, husababisha utata.
Alisema waendesha pikipiki wa kawaida wanawaharibia wanaofanya biashara halali wanaobeba abiria.
Alisema Uwapa hawajapanga maandamano na walipata taarifa kutoka kwa watu binafsi na walishtushwa kusikia kuna maandamano hayo. Rugemalila alisema wanaendelea kufanya utafiti kwa kushirikiana na polisi ili kufahamu ni waliohusika kuratibu maandamano hayo.
Aliwashauri waendesha bodaboda wafuate sheria za usalama barabarani kama zinavyoelekeza, wahakikishe wana leseni, kofia ngumu na waegeshe pikipiki kwenye vituo vilivyosajiliwa.
Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo, waendesha bodaboda waliosajiliwa na wanaotambulika na Uwapa hadi sasa ni 2,950, vituo vilivyosajiliwa ni 144 na vituo bubu vinavyotarajiwa kusajiliwa karibuni ni 55.
CHANZO ; HABARI LEO.

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa