Home » » MUSTAFA PANJU AJINADI KWA WANANCHI WA JIMBO LA ARUSHA ASEMA AKIPATA UBUNGE HAWATAJUTIA KAMWE‏

MUSTAFA PANJU AJINADI KWA WANANCHI WA JIMBO LA ARUSHA ASEMA AKIPATA UBUNGE HAWATAJUTIA KAMWE‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
SAM_3941Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Bushbucks Safaris iliyopo jijini Arusha Mustafa Panju ambaye ni mmoja wa wagombea wa jimbo la Arusha mjini kupitia chama cha mapinduzi CCM akiongea katika mkutano wa hadhara katika kata mpya ya Olmoti jana ambapo wagombea 12 walipata fursa ya kujitambulisha kwa wananchi na kunadi sera zao, Mustapha panju amesema kuwa kilicho msukuma kugombea nafasi hiyo ni kuakikisha wananchi wa jimbo la arusha wanapata ridhaa ya kuwa na maendeleo ya hali ya juu ikiwemo kuweza kukua kisayansi na kuweza  kufika mwezini.(Habari Picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)
SAM_3903Mustafa Panju akiwa na wagombea wenzake wa chama hicho jana katika kata mpya ya Olmoti jijini Arusha walipokwenda kujitambulisha kwa wananchi na kunadi sera zao pia walipata fursa ya kutembelea kata ya Olasiti,Osunyai JR
SAM_3972Mtoto aliyefika kusikiliza sera za wagombea Ubunge wa chama cha Mapinduzi (CCM) akiwa ameshikilia kipeperushi cha mgombea Ubunge jimbo la Arusha Mustafa Panju katika kata ya Osunyai JR
SAM_3905Katibu wa CCM wilaya ya Arusha, Ferooz Bano akizungumza katika kata mpya ya Olmoti jana ambapo alisisitiza wananchi kusikiliza sera za wagombea huku akiwataka kutokupiga makofi au kushangilia wakati wakijieleza
SAM_3918Meza kuu pamoja na wagombea Ubunge jimbo la Arusha mjini
SAM_3974Wananchi waliokuja kuwasikiliza wagombea Ubunge jimbo la Arusha mjini wakiwa makini kusikiliza,

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa