Ujumbe wa wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya NHC ukiwa eneo
linalomilikiwa na NHC ambalo ujenzi wa
Mji wa kisasa umeanza wakionyeshwa na Meneja wa NHC Mkoa wa Arusha Bw. James
Kisarika chemchemu za maji yanayotiririka walipotembelea eneo hilo lenye hali
ya hewa ya aina yake Jijini Arusha jana.
Usariver ni Arusha Tanzania ambapo NHC Shirika lenye dhamana ya kujenga
nyumba bora hapa nchini limeanza kupanga mji huo wenye mandhari na hali ya hewa
ya kuvutia. Hapa wajumbe wa Bodi ya NHC na watendaji wa NHC wanafurahia mpango
wa kuendeleza eneo hilo lenye ekari 300 linalomilikiwa na NHC.
Hii ndiyo hatua ya ujenzi iliyokwishafikiwa hivi sasa katika ujenzi wa
nyumba za gharama ya kati aina ya “town houses” zinazojengwa na NHC Wilayani
Monduli kwa ajili ya watumishi wa Halmashauri hiyo.
Kaimu Mkurugenzi wa Uendelezaji Miliki wa NHC, Bw. Haikamen Mlekio
akitoa maelezo ya awali kwa Makamu Mwenyekiti wa NHC Bw. Deo Mmari na wajumbe
wengine wa Bodi, ya utekelezaji wa ujenzi wa nyumba za gharama ya kati aina ya
“town houses” zinazojengwa na NHC Wilayani Monduli kwa ajili ya watumishi wa
Halmashauri hiyo.
Msimamizi wa mradi wa nyumba za gharama ya kati zinazojengwa na NHC
Wilayani Monduli Bw. Hassan Bendera(kushoto) akitoa maelezo kwa Makamu
Mwenyekiti wa NHC Bw. Deo Mmari(mwenye suti nyeupe), ya hatua za ujenzi
zilizofikiwa katika mradi wa nyumba za watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya
Monduli zinazojengwa na NHC
Meneja wa NHC Mkoa wa Arusha Bw. James Kisarika akitoa maelezo kwa
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NHC Bw. Deo Mmari ya viwanja
vilivyotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Monduli ambavyo hivi karibuni
vitajengwa nyumba za gharama nafuu. Eneo
hili limepewa NHC na Halmashauri hiyo kama sehemu ya kulipa gharama
zilizotokana na NHC kuijengea Halmashauri hiyo nyumba za watumishi wake.
Meneja wa NHC Mkoa wa Arusha Bw. James Kisarika akitoa maelezo ya
mpango wa uendelezaji mji wa kisasa wa Safari City ulioko Mateves nje kidogo ya
Jijini Arusha mbapo hivi karibuni NHC itaanza ujenzi wa nyumba 300 za gharama
nafuu za kuuzia wananchi.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NHC Bw. Deo Mmari na
Wakurugenzi wengine wa Bodi wakijadili jambo kuhusu mpango mji uliyowekwa na
NHC katika uendelezaji wa mji mpya wa Safari City wenye ekari 600 alipotembelea
eneo hilo lililopo Mateves nje kidogo ya Jiji la Arusha jana.
Meneja Msimamizi wa mradi wa ujenzi wa nyumba na vivutio mbalimbali
katika eneo la NHC Usariver Bw. Muradi Yusufali akiwatembeza Wajumbe wa Bodi ya
Wakurugenzi ya NHC katika mradi wa ujenzi wa mji wa kisasa Usariver
walipotembelea eneo hilo jana. Ukamilishaji taratibu kadhaa za ujenzi wa nyumba
katika eneo hilo na ujenzi wake umeshaanza.
Meneja wa NHC Mkoa wa Arusha Bw. James Kisarika akiwapa wajumbe wa Bodi
ya Wakurugenzi maelezo na mpango wa uendelezaji wa mji wa kisasa eneo la
Usariver lenye vivutio kadhaa walipotembelea eneo hilo lenye ekari 300 jana.
.png)
.png)
.png)
.png)
.png)
.png)
.png)
.png)
.png)

0 comments:
Post a Comment