Immaculate Makilika –MAELEZO ARUSHA
Rais wa Shirikisho la
Ujerumani amesema Serikali yake iko tayari kushirikiana na Mahakama ya
Afrika katika utendaji kazi wake ili kusaidia
kutoa huduma iliyokusudiwa kwa walengwa.
Rais huyo
ameyasema hayo leo alipotembelea Mahakama ya
Afrika iliyopo mjini Arusha,
ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya siku sita nchini na kusema kuwa angependa
kuona utawala wa sheria ambao
unaozingatia demokrasia unafuatwa na
kuheshimiwa.
Aidha, Rais Ghauck ameipongeza mahakama hiyo kwa
weledi wake na hatua nzuri waliyofikia huku akitolea mfano kesi iliyosikilizwa
mwaka 2014 huko Adis Ababa, Sudan.
‘Tunaunga mkono
maendeleo pia tungependa kuendelea
kushirikiana nanyi, msisite kutuomba msaada alisema Rais Gauck’.
Naye kwa upande
wake Jaji Mkuu wa Mahakama ya Afrika Augustino Ramadhani alisema Serikali ya Ujerumani imekua na
ushirikaiano mzuri na Mahakama hiyo kwani ilisaidia pia katika ujenzi wake.
Hata hivyo jaji
Ramadhani amesema wamemuomba Rais wa Ujerumani asaidie kujenga mahakama ya
Afrika ya Mashariki, ombi ambalo Rais huyo amesema atalishughulikia
kushirikiana na viongozi aliongozana
nao.
Aidha, Jaji
Ramadhani amesema kuwa uwepo wa Mahakama hii Afrika ni jambo la kujivunia kwani itaweza kusaidia matatizo ya waafrika
wote kutoka sehemu mbalimbali.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment