Home » » Jamii yatakiwa kutoa kipaumbele kwa vijana wakati wa mipangilio ya bajeti zao

Jamii yatakiwa kutoa kipaumbele kwa vijana wakati wa mipangilio ya bajeti zao


Na Mwandishi Wetu, Arusha
Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniella Schadt ametoa wito kwa jamii kuhakiksha wanatoa kipaumbele katika kushirikisha vijana kwenye nyanja mbalimbali za maendeleo.
Wito huo umetolewa juzi jijini Arusha wakati Mke huyo wa Rais wa Ujerumani alipokuwa akizindua mradi wa utetezi na ushawishi wa jamii katika kutoa vipaumbele katika sekta za Elimu, Afya na Ajira kwa vijana ujulikanao kama BEYOND 2015 ambapo mradi huo unaratibiwa na Shirika lisilo la Kiserikali la DSW Tanzania.
Bibi. Daniela alisema kuwa jamii inapaswa kutoa mkazo katika sekta za Elimu, Afya na Ajira kwa vijana kwa kuwa duniani kote vijana ndiyo nguvu kazi katika kuletea maendeleo ya taifa lolote lile.
‘Tunapaswa kuweka mkazo kwa vijana wadogo, maisha yao ya baadaye yanaanza kuanzia sasa, tuweke mkazo katika Elimu na Afya kwa vijana wetu ili waeze kutambua fursa na kuzitumia.’’ Alisema   Bibi. Daniela.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa DSW Tanzania Bwana Peter Owaga amesema kuwa ni wao kama asasi ya kirai wanashirikia na Serikali katika kuhakikisha utekelezaji wa sera zinazohusu vijana nchini zinaleta tija
Owaga ameongeza kuwa Serikali kama msimamizi imepiga hatu kubwa kwa kuwa na Sera na miongozo mbalimbali inayohusu vijana kama vile Sera ya Maendeleo ya Vijana ya mwaka 2007 inayotoa fursa kwa kijana kujitambua.
Aidha Owaga aliongeza kuwa mradi wa BEYOND 2015 ambao umezinduliwa na Mke wa Rais wa UjerumaniBibi. Daniela Schadt umelenga kuongeza ushawishi na hamasa kwa washirika wa maendeleo ili kutoka kipaumbele kwa kutenga bajeti kwa ajili ya Elimu , Afya ya Uzazi na Ajira kwa vijana.
Akizungumzia mikakati na namna mradi huo utakavyotekelezwa Afisa Muhamasishaji na Mawasiliano Bi. Ester Mwanjesa amesema kuwa mradi huo utatekelezwa kwa mwaka mmoja katika mikoa yote nchini ambapo mijadala mbalimbali itakuwa ikifanyika ili kuongeza hamasa ya uashawishi utakaopelekea kutoa kipaumbele kwa vijana hususan katika nyanja za Elimu, Afya ya uzazi na Ajira.
Mradi huu wa BEYOND 2015 ambao ni kifupi cha maneno Building Expert Youth and Organisation for National Postion on the Post 2015 Development umelenga kutatua changamoto za vijana asa baada ya kumalizika kwa muda wa Malengo ya Melenia mapema mwaka huu.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa