Arusha
Home » » 'TUMIENI VYAKULA VYENYE VIRUTUBISHO'

'TUMIENI VYAKULA VYENYE VIRUTUBISHO'

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WATANZANIA wameshauriwa kutumia vyakula vyenye virutubisho badala ya kula vilivyokobolewa, hali inayochangia watu wengi kudhoofika kiafya na kupata magonjwa ikiwemo utapiamlo.
Meneja Masoko wa Kampuni ya Monaban inayojihusisha na usambazaji wa vyakula vyenye virutubisho ndani na nje ya nchi, George Mboje, alitoa kauli hiyo mjini hapa hivi karibuni na kusema kukosekana kwa  virutubisho muhimu katika vyakula kumekuwa kukisababishia watu kushambuliwa na maradhi kwa urahisi.
Kutokana na hali hiyo, aliwashauri Watanzania kutumia bidhaa zisizokobolewa zenye virutubisho, ili kujenga jamii imara yenye afya bora itakayoleta uchumi imara kuanzia ngazi ya familia hadi taifa.
“Kwa sasa wazalishaji wote wamepokea maelekezo kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) juu ya kuongeza virutubisho kwenye vyakula, sisi ni wadau ambao tunatekeleza maagizo hayo na kuwatendea haki walaji kwa kuwauzia vyakula vyenye virutubisho,” alisema George.
Alisema kampuni hiyo imekuwa ikisambaza vyakula vyenye virutubisho ndani na nje ya nchi ambavyo ni unga wa mahindi, ngano, maharage na nafaka nyingine.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa