Mkuu wa mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo
Kufuatia tukio hilo serikali mkoani Arusha imepiga marufuku
uchimbaji wa kokoto katika eneo hilo na kuagiza kamati iliyoundwa mwaka
jana baada ya ajali kama hiyo kutokea katika eneo la Moshono kufanya
uchunguzi katika migodi yote.
Mkuu wa mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, ametoa amri hiyo baada ya
kufika katika eneo la tukio na kuongea na viongozi wa eneo hilo.
Kwa mujibu wa Mulongo kamati hiyo itatakiwa kuleta mapendekezo ya namna ya kuboresha hali ya usalama katika machimbo.
“Ile kamati sasa itaanza upya kuchunguza hali ya usalama na kuleta mapendekezo ya kuhakiki hali ya usalama,” alisema Mulongo.
Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi mkoa wa
Arusha, Liberatus Sabas, aliwataja waliopoteza maisha kuwa ni Joseph
Solomon (18) na Saimon Petro (15), wote wakazi wa Muriet.
Katika hatua nyingine jeshi la polisi mkoani Arusha kupitia kwa
kamanda Sabas limewataka watu wanaomiliki migodi ya uchumbaji wa kokoto
kuhakikisha kuwa wana vibali vya kufanya kazi hiyo.
“Tunapiga marufuku haya machimbo yanayoanzishwa kiholela na
kuhatarisha maisha ya watu, tutaanza kufuatilia na kuchukua hatua kwa
kushirikiana na vyombo vingine vya serikali,” alisema Sabas.
Aliongeza kuwa pia katika migogodi hiyo wahakikishe kuwa kuna usalama wa kutosha ikiwemo miundombinu ya tahadhari na uokoaji.
Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa lilitokea saa 3 asubuhi jana
katika machimbo hayo baada ngema kuwaangukia vijana waliokuwa wakichimba
na kupakia moram katika gari lililofika katika machimbo hayo.
“Lilitokea ghafla sana mimi nilikuwa juu mara nikasiakia ngema
inakatika yaani nilishuhudia wenzangu wakifunikwa na udongo na kupoteza
maisha,” alisema manusura Loiruk Sandamu.
Tukio hilo ni la pili kutokea katika machimbo ya kokoto jijijni
Arusha baada ya Machi 16, mwaka jana kuanguka na kufukia watu 16 katika
eneo la Moshono.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment