Home » » 2015 kila Mtanzania kuwa na anuani ya makazi

2015 kila Mtanzania kuwa na anuani ya makazi



na Ramadhani Siwayombe, Arusha

SEREKALI imesema hadi kufikia mwaka 2015 kila Mtanzania atakuwa na anuani ya posta ya makazi kupitia mpango maalumu unaoendelea wa kuandika namba za nyumba na mitaa kote nchini.
Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, alibainisha hayo jana wakati akifungua mkutano wa 32 wa mwaka wa muungano wa mashirika ya posta Afrika (PAPU).
Alisema mpango huo unaendana sambamba na dira ya taifa ya mwaka 2015 ambayo imeanisha vipaumbele mbalimbali ikiwamo hiyo ya kuwapatia wananchi anuani zitakazowarahisishia kufikiwa na huduma mbalimbali za maendeleo.
Alisema kuwapo na anuani za uhakika kwa wananchi ni sehemu mojawapo muhimu ya kupanga mipango ya maendeleo kwa wananchi kwa kuwafikishia huduma muhimu za kijamii katika maeneo yao kulingana na mahitaji.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), John Mkoma, alisema tayari anuani za makazi kwa nchi nzima Zimekwisha kuandaliwa na kukamilika, hivyo hivi sasa jukumu lililopo ni kuzisambaza pekee.
Mkoma alisema anuani hizo zilikwisha kupitishwa na serikali na kutangazwa katika gazeti la serikali la Juni 22, mwaka 2012, hivyo kuwa sheria.
Awali, akizungumza katika ufunguzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Universal Posta Union, Balozi Bisher Husein, alizitaka serikali za nchi za Afrika kusaidia mashirika ya posta ya nchi zao kwa kuwa yanafanya kazi kubwa kuwahudumia wananchi wa vipato vya chini.

CHANZO TANZANIA DAIMA 

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa