Habari
zilizotufikia hivi punde chumba cha habari cha mtandao huu, zinasema
kuwa Hali si shwari katika jiji la Arusha, ambapo hadi muda huu bado
mabomu ya machozi yanaendelea kurindima baada ya Askari Polisi kuanza
zoezi hilo kwa ajili ya kuwatawanya watu wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa
CHADEMA, waliokusanyika katika viwanja vya Soweto wa ajili ya maombolezo
ya watu waliofariki katika tukio la mlipuko wa bomu lililotokea
mwishini mwa wiki iliyopita katika mkutano wa Chadema.
Aidha
imeelezwa kuwa awali watu hao walizuiliwa kukusanyika eneo hilo na
baadaye viongozi wa chadema walipofika eneo hilo walianza kuwahutubia
wananchi waliokusanyika eneo hilo jambo ambalo lilizuiliwa huku vijana
wakiimba nyimzo za maombolezo na za siasa, jambo lililowafanya askari
kuchukua jukumu la kuwatawanya kwa mabomu ya machozi.
WAKATI HUO HUO:- habari zinaendelea kusema kuwa Mbunge wa Mbeya mjini JOSEPH MBILINYI Mr. ii, SUGU, amenusurika kufa baada ya kupata ajali eneo la Katesh Wilaya ya AHanang mkoa Manyara wakati akiwa njiani kuelekea jijini ARUSHA.
Polisi Mkoa wa Arusha inawashikilia baadhi ya Viongozi wa CHADEMA, Mbunge
wa Singida Mashariki Tundu Lisu na viongozi wengine kwa kuitisha
mkutano usiokuwa halali ili kuondoa uvumi wa kuwa mbunge amefariki
Dunia.
CHANZO : SUFIANI MAFOTO BLOG
0 comments:
Post a Comment