Home » » TCAA YAANZA KUCHUNGUZA CHANZO CHA AJALI YA NDEGE ARUSHA

TCAA YAANZA KUCHUNGUZA CHANZO CHA AJALI YA NDEGE ARUSHA

Mamlaka ya viwanja vya ndege nchini TCAA imeanza kufanya uchunguzi wa kitaalamu kubaini chanzo cha ajali ya ndege iliyotokea mkoani  Arusha jana na kusababisha kifo cha rubani wake.
Ndege hiyo ndogo  yenye uwezo wa kubeba kati ya watu 4 hadi sita ilianguka juzi jioni majira ya saa 12:45 wakati ikajaribu kutua kwenye uwanja wa ndege wa arusha.
Aliyefariki katika ajali hiyo  ametambuliwa kuwa ni mfanya biashara maarufu  wa  wa mjini moshi  Joseph Malya almaarufu kwa jina la Bob Sambeke.
Meneja wa  mamalaka ya viwanja vya ndege  mkoani  Arusha   Bwana Aswile    Kamendu amewaambia waandishi wa habari kuwa  ofisi yake inasubiri mtaalamu kutoka wizara ya uchukuzi  ili kuendelea na uchunguzi wa kina uliosababisha ajali hiyo ya ndege.
Taarifa za awali zilizowakariri mashuhuda zinadokeza kuwa ndege hiyo ilipoteza mawasiliano kisha ,kuanguka  kando ya mti mkubwa  eneo la magereza mita 200 kutoka barabara ya kurukia ndege katika uwanja  huo.
Mapema jana jioni ndugu wa marehemu  Mallya  waliokuwa katika harakati za kusafirisha mwili wake kutoka hospitali ya mkoa wa arusha mount Meru hadi mjini moshi kusubiri taratibu za maziko.
Ajali za ndege katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro zimekuwa zikiripotiwa kuongezeka ambapo jumla ya ndege 4 na helkopita moja zimeanguka katika kipindi cha miaka saba iliyopita na kusababisha vifo,majeruhi na uharibifu mkubwa wa mali

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa