Home » » WANACHAMA LAPF KUANZA KUTUMIA KADI

WANACHAMA LAPF KUANZA KUTUMIA KADI

na Grace Macha, Arusha
MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Serikali za Mitaa (LAPF) unabadili mfumo wake wa huduma ili uendane na ule wa kibenki ambapo utawawezesha wanachama kutumia kadi wakati wa kudai mafao yao tofauti na sasa ambapo hutakiwa kuwa na nyaraka mbalimbali ikiwemo barua ya ajira.
Aidha, mfuko huo unaanzisha mfumo utakaowawezesha wanachama kupata taarifa za michango yao kupitia simu zao za kiganjani, hivyo kuwaondolea usumbufu wa kulazimika kwenda zipata kwenye matawi yao.
Hayo yalibainishwa mwishoni mwa wiki mjini hapa na Mkurugenzi Mkuu wa LAPF, Eliudi Sanga, alipozungumza na waandishi wa habari juu ya maandalizi ya mkutano wao mkuu wa tano unaotarajia kuanza leo ambao kaulimbiu yake ni ‘Hifadhi ya jamii na ukuaji wa uchumi’.
Alisema maboresho hayo ni mwendelezo wa malengo ya mfuko huo katika kuhakikisha wanachama wake wananufaika zaidi kwa kuwawezesha kumudu maisha kabla na baada ya kustaafu.
“LAPF ni mfuko pekee wa kijamii ambao wanachama huchangia kiasi kidogo cha asilimia 5 ya mshahara wao huku waajiri wakichangia asilimia 15 tofauti na mifuko mingine ambayo mwanachama huchangia asilimia 10 na mwajiri asilimia 10, tunataka mwanachama amudu maisha, atunze familia yake vizuri, aweze kuwasomesha watoto wake,” alisema Sanga.
Chanzo: Tanania Daima

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa