Home » » MAONESHO YA UTALII YA KARIBU TRADE FAIR KUANZA IJUMAA HII JIJINI ARUSHA

MAONESHO YA UTALII YA KARIBU TRADE FAIR KUANZA IJUMAA HII JIJINI ARUSHA

 Katibu mtendaji TATO, Mustapha Akunaay akiongea na waandishi wa habari
 Mjumbe wa kamati ya maandalizi Andrew Malalika
Baadhi ya mabanda katika uwanja wa Magereza yakiwa tayari kwa kazi

Na Idd Uwesu- Arusha Yetu
******************
Maonesho ya kimataifa ya Karibu Trade Fair yanatarajiwa kuzinduliwa ijumaa hii huku Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mh. Lazaro Nyarandu akitarajiwa kuyazindua rasmi jijini Arusha
Maonesho hayo ambayo ni ya 12 na yaliyokuwa yafanyike mwishoni mwa mwezi wa tano na kuahirishwa ili kupisha Mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika yatafanyika katika viwanja vya Magereza jijini humo.
Akiongea na waandishi wa habari katibu mtendaji  wa chama cha watoa huduma  za utalii Tanzania TATO ambao ndio waandaaji wa maonesho hayo Mustapha Akunaay, amesema maandalizi kwa ajili ya maonesho hayo yamekamilika kwa kiasi kikubwa huku wakiwa wamefanya maboresho makubwa  ya miundo mbinu na huduma muhimu uwanjani hapo.
Ameongeza kuwa maonesho haya ambayo ni ya pili kwa ukubwa barani Afrika baada ya yale ya Indaaba ya Afrika kusini, mwaka huu yamepata washiriki wapya kutoka nchi za brazil, Norway na china. 
Nae  mjumbe wa kamati ya maandalizi Andrew Malalika amesema bonanza linalohusisha michezo mbalimbali ambalo huandaliwa sambamba na  maonesho hayo litafikia tamati siku ya ijumaa katika viwanja vya General tyre vilivyoko Njiro jijini hapa na kuongeza kuwa michezo mbalimbali itahusishwa ikiwemo mpira wa miguu, kuvuta kamba na kukimbiza kuku.
Maonesho hayo yanayofanyika kila mwaka yana lengo la kuwakutanisha wadau wa sekta utalii nchini na wale wanouza utalii kutoka nje ya nchi ili kuhamasisha maendeleo ya sekta hiyo nchini. Maonesho hayo mwaka huu yatashirikisha washiriki 265 kati yao 33 ni kutoka  nje ya nchi.
MWISHO.

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa