Arusha
Home » » ARUSHA MERU YAKOPESHA AKINAMAMA MILIONI 151/-

ARUSHA MERU YAKOPESHA AKINAMAMA MILIONI 151/-

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 

ZAIDI ya mikopo ya sh. milioni 151 imetolewa kwa akinamama 287 kwa muda wa miaka mitatu tangu mwaka 2012 hadi 2014 na kikundi cha Arusha Meru Women Saccos lengo ikiwa ni kuwainua akinama kuichumi.

Hayo yalisemwa na mwenyekiti wa kikundi hicho Bi.Eva Kaaya juzi katika maonyesho ya Nanenane katika Viwanja vya Themi jijini Arusha.

Alisema kuwa hadi sasa wametoa mikopo kwa akinamama zaidi ya sh.milioni 151 kwa ufadhili wa Canadian Co-operative Association kupitia Moshi University College of Co-operative and Business Studies.

Alisema kuwa lengo lao hasa la kufanya hivyo ni kuwainua akinamama kiuchumi hali itakayopelekea wao kuondokana na umaskini katika familia zao huku akiweka wazi kuwa hadi sasa mikopo iliyorejeshwa ni sh. milioni 97,644,066 na mikopo iliyobaki ni sh.milioni 53,735,934.

Bi.Kaaya alisema kuwa wamekuwa wakiwahudumia akinamama kutoka Arusha na Arumeru kwa kuwapa mikopo wajasiriamali, ambapo sharti la kupata mkopo ni lazima awe na hisa katika kikundi hicho na kumfanya mwombaji wa mkopo awe mmiliki halali wa Saccos.

"Ili akinamama wapate mkopo ni lazima wawe katika kikundi cha watu watano,awe mwanachama hai na awe na akiba kwa kufuata masharti hayo mwombaji anapewa mkopo bila ya msharti magumu," alisema Bi.Kaaya.

Kwa upande wake katibu wa kikundi hicho Bi. Martha Temba alisema kuwa njia mojawapo iliyowafanya wakafika hapo ni utoaji wa mafunzo kwa akinamama juu ya elimu ya Saccos kwa kuweka na kukopa inayotolewa na Chuo cha Ushirika Moshi.

"Mafanikio tuliyonayo sasa ni kutokana na akinamama kupewa elimu ya Saccos,kabla ya elimu walikuwa wakichukua mikopo kienyeji hali iliyopelekea wengine kushindwa kuendelea na kikundi," alisema Bi.Temba.

Aidha, alisema kuwa wapo na timu kutoka ushirika ambapo wanawafikia kina mama katika kata na vijijini na kuwapa elimu ya Saccos.

Naye Afisa Ushirika Halmashauri Wilaya ya Arusha DC Bi.Sophia Shoko alisema kuwa majukumu yao makubwa ni kusimamia sheria na kukagua,kuhamasisha wanachama kujiunga katika Saccos.

Pia aliongeza kuwa kazi yao ni pamoja na utoaji elimu ya ushirika, utunzaji wa kumbukumbu,haki na wajibu wa mwanachama,huku akiwataka akinamama kupunguza kuwa na mikopo mingi isiyokuwa na tija

Chanzo:Majira

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa