Arusha
Home » , » SOKOINE MINI MARATHON 2014: Usajili wa namba za washiriki umeanza rasmi

SOKOINE MINI MARATHON 2014: Usajili wa namba za washiriki umeanza rasmi


Namba zimeanza kutolewa kwa washiriki wa mbio za Sokoine Mini Marathon Km 21 na Km 2 ambazo zitatimua vumbi Aprili 12, 2014 Monduli mkoani Arusha, rais Jakaya Kikwete ndiye atakayepuliza kipenga cha kuanza mbio hizo.

Ada ya namba ni Tsh: 2,000 tu, namba zinapatikana Arusha pale Uwanja wa kumbukumbu ya SHEIKH AMRI ABED KARUME na Monduli pia.

Kwa washiriki wote nje ya mkoa wa Arusha wasiliana na VICTOR MACHOTA kwa 0787415864 ambaye atapokea usajili kwa njia ya simu na namba yako utajulishwa kwa SMS na itahifadhiwa hadi utakapoichukua. Mwisho wa kuchukua namba yako ni Ijumaa April 11, 2014 Arusha mjini.

Kwa wale watakaosajili kwa njia ya simu tunaomba mtume hela kwa AIRTEL MANEY kwa namba ya Victor Machota, unaombwa uongezee gharama kidogo ya kutoa pesa mtandaoni.

Kwa wale watakaosajili namba papo kwa papo wawasiliane na PHAUSTIN BAHA 0753860668 kwa maelezo zaidi na kwa wale wa Monduli wawasiliane na ROBERT MOLEL kwa 0753739128.

Kwa ratiba kamili hapo baadae pitia blogu zifuatazo; WOTE MNAKARIBISHWA KUSHIRIKI NA RAIS WA JAMHURI YA TANZANIA.

-          wazalendo25.blogspot.com
 
-          victormachota.blogspot.com

-          gidabuday.blogspot.com




Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa