Arusha
Home » » Bakwata yataka wa mazingira magumu wasaidiwe

Bakwata yataka wa mazingira magumu wasaidiwe

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) mkoani hapa, limeitaka jamii nchini kuhakikisha inaangalia familia zilizoachwa na wazazi wao na kuishi kwenye mazingira magumu zisaidiwe ziweze kujikimu kimaisha.
Hayo yalisemwa jana na Mwenyekiti wa Bakwata Mkoa wa Arusha, Shehe Mohamed Maviwa wakati akikabidhi msaada wa vifaa vya ushonaji kwa msichana Amina Mohamed (20) wa Sombetini anayetokea katika familia inayoishi kwenye mazingira magumu.
Alisema ni jukumu la jamii kuhakikisha inazisaidia jamii zenye mahitaji maalumu kwani zimekuwa zikikabiliwa na changamoto mbalimbali na mwisho wa siku watoto kujiingiza kwenye makundi yasiyofaa.
“Kuna jamii nyingi ambazo zinakabiliana na changamoto mbalimbali kutokana na familia nyingi kuathirika kwa kuachwa na kubakia masikini hatua ambayo inachangia watoto kuishia kukaa mtaani kujiingiza kwenye makundi yasiyofaa,” alisema Maviwa.
Naye Katibu wa Bakwata Mkoa wa Arusha, Abdalah Masood alisema wamefikia hatua ya kumsaidia mtoto huyo kutokana na changamoto zinazomkabili ikiwamo kuwa na jukumu la kulea wadogo zake na mama yake.
“Naiomba jamii isaidie jamii zenye mahitaji kama hizi kwani zimekuwa na changamoto nyingi kutokana na kukosa msaada,” alisema Masood.
Kwa upande wake, Amina aliwashukuru kwa msaada huo kutokana na changamoto mbalimbali zilizokuwa zikimkabili ikiwamo ukosefu wa vifaa vya ushonaji pamoja na kuwa na ujuzi huo.
Alisema, bado anakabiliwa na changamoto ya sehemu ya kushonea hivyo aliomba wadau mbalimbali kumsaidia ili aweze kupata eneo na hatimaye kuendeleza biashara yake.
Chanzo Gazeti la Habari leo
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa