Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Umoja
wa Watanzania wanaofanyakazi wa Jumuiya ya Afrika
Mashariki(WATJAM)yenye makao yake makuu jijini Arusha wakiwasili kwenye
hospitali ya halmashauri ya wilaya ya Meru kufanya usafi na kutoa
misaada mbalimbali kwaajili ya kuadhimisha Siku kuu ya Muungano wa
Tanzania leo.
Watanzania
wanaofanyakazi kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki(EAC)yenye makao yake
makuu jijini Arusha wakifanya usafi kuzunguka mazingira ya hospitali
hiyo leo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 51 ya muungano wa
Tanganyika na Zanzibar.
Mganga
Mkuu wa hospitali ya halmashauri ya wilaya ya Meru,Arusha,Dk Azizi
Msuya(kushoto)akipokea sehemu ya zawadi zilizotolewa na Wafanyakazi wa
EAC ambao ni Watanzania kutoka kwa Mwenyekiti wa umoja huo,James Kuleiye
yenye thamani ya Sh.3.7 milioni.
Na Mwandishi Wetu
Umoja
wa Watanzania wanaofanyakazi wa Jumuiya ya Afrika
Mashariki(WATJAM)yenye makao yake makuu jijini Arusha katika
kuhadhimisha Sikukuu ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar leo
wametembelea hospitali ya halmashauri ya wilaya ya Meru kufanya usafi
na kutoa misaada mbalimbali yenye thamani ya zaidi ya Shilingi 3.7
milioni
Mwenyekiti
wa umoja huo,James Kuleiye amesema wao kama watanzania wameona waitumie
siku ya leo kufanya shughuli za kijamii na kuwa karibu na taasisi hiyo
kwa lengo kujenga mahusiano mema.
Misaada
iliyotolewa ni Maji maluumu ya wagonjwa ,Mashuka 50,Vifaa tiba vya
kupima mapigo ya moyo(Presha) na vifaa mbalimbali vya usafi.
Mganga
Mkuu wa hospitali hiyo,Aziz Msuya ameshukuru umoja huo kwa moyo wa
uzalendo na kuzitaka taasisi nyingine kuiga mfano huo licha ya kueleza
changamoto inayoikabili hospitali hiyo ya kutokuwa na Wodi ya kuwalaza
wagonjwa waliofanyiwa Upasuaji.
Amesema
vifaa hivyo vitakua msaada mkubwa kuboresha afya ya mama na mtoto kwani
kila mwezi jumla ya wanawake 300 hujifungua huku 50 wakijifungua kwa
upasuaji.
Kwa hisani ya Michuzi Media
0 comments:
Post a Comment