Arusha
Home » » MAKAMU WA RAIS DKT GHARIB BILAL AFUNGUA MKUTANO WA KWANZA WA KIMATAIFA KATIKA BARA LA AFRIKA, WENYE LENGO LA KUTANGAZA UTALII WA NCHI ZA AFRIKA.

MAKAMU WA RAIS DKT GHARIB BILAL AFUNGUA MKUTANO WA KWANZA WA KIMATAIFA KATIKA BARA LA AFRIKA, WENYE LENGO LA KUTANGAZA UTALII WA NCHI ZA AFRIKA.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia alipofungua Mkutano wa kwanza wa  Kimataifa wa Kutangaza Utalii kwa Nchi za Bara la Afrika na Kuhamasisha Utalii Endelevu katika nchi hizo.  Mkutano huo umefunguliwa leo Oktoba 15, 2012 katika Ukumbi wa AICC  leo Oktoba 15 Jijini Arusha na kuhudhuriwa na mawaziri 17 kutoka nchi mbalimbali za Afrika.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (kushoto) akipokea barua ya wazi kutoka kwa Katibu wa Mkuu wa Shirika la Utalii la Dunia, Taleb Rifai, iliyotolewa na Baraza la Waendesha Utalii Duniani (WTTC) mara baada ya kufungua Mkutano wa Kuhamasisha utalii barani Afrika leo, Oktoba 15, 2012, jijini Arusha. Katika Mkutano huo pia umehudhuriwa na Mawaziri 17 kutoka nchi mbalimbali za Afrika.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia Pakti ya kifuko cha unga wa Ubuyu na kusikiliza maelezo kutoka kwa Meneja Masoko na Mauzo wa kampuni ya Moringa Consultancy (TZ) Co Ltd, Christina
 Ngoti, wakati Makamu alipokuwa akitembelea Mabanda ya Maonyesho baada ya kufungua mkutano wa kwanza wa  Kimataifa wa Kutangaza Utalii kwa Nchi za Bara la Afrika na Kuhamasisha Utalii Endelevu katika nchi hizo. Mkutano huo umefanyika leo Oktoba 15, 2012 jijini Arusha.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mtaalam wa Tiba za Asili, James Kangaa, wakati Makamu alipokuwa akitembelea Mabanda ya Maonyesho baada ya kufungua mkutano wa  kwanza wa  Kimataifa wa Kutangaza Utalii kwa Nchi za Bara la Afrika na Kuhamasisha Utalii Endelevu katika nchi hizo. Mkutano huo umefanyika leo Oktoba 15, 2012 jijini Arusha.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipunga mkono kuwaaga wasanii wa ngoma ya asili wa kabila la kimasai wakati akiondoka katika ukumbi wa mikutano wa AICC jijini Arusha leo Oktoba 15, 2012 baada ya kufungua mkutano wa kwanza wa Kimataifa wa Kutangaza Utalii kwa Nchi za Bara la Afrika na Kuhamasisha Utalii Endelevu katika nchi hizo.Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa