na Ramadhani Siwayombe, Arusha
MAPIGANO
mapya yaliyoibuka kati ya wafugaji wa jamii ya Kimasai na wa Kiarusha katika
kijiji cha Engarenaiboi wilayani Longido, yamesababisha watu tisa kujeruhiwa
vibaya na kukimbizwa hospitalini.
Mapigano
hayo yaliibuka juzi kutokana na mgogoro wa malisho uliokuwa ukiendelea kati ya
pande hizo mbili katika eneo la mpaka wa wilaya za Longido na Arumeru katika
kijiji cha Kiseriani.
Mgogoro
huo unatokana na wafugaji wa Kiarusha wenye asili ya wilaya ya Arumeru
wanaoishi katika kijiji cha Kiseriani kilichoko wilaya ya Longido kuhitilafiana
juu ya eneo la malisho ya mifugo na wafugaji wa Kimasai wa asili ya Longido.
Akizungumzia
mgogoro huo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, alisema baada ya wao juzi
kwenda kutatua mgogoro wa Kiseriani kwa kuwasihi wafugaji hao kuacha dhana ya
ubaguzi waliyoianzisha kati yao, ndipo kukazuka tena mapigano katika kijiji cha
Engarenaibor.
Mulongo
alisema baada ya kupata taarifa za kuzuka kwa mapigano hayo walituma askari na
walifanikiwa kudhibiti mapigano hayo na kukuta tayari watu hao tisa
wamejeruhiwa.
Mkuu
huyo wa mkoa alitoa wito kwa jamii hizo kuacha tabia wanayotaka kuianzisha ya
kutengana kwa ukabila, kwani itawaathiri kwa kuwa wana tabia ya kuhama kufuata
malisho.
“Nimewaambia
wasipoacha dhambi hiyo ya kubaguana wao ndio watakuwa waathirika wakubwa wa
dhambi hiyo kwa kuwa ndio wako katika mikoa mingi hapa nchini wakifuata malisho
hivyo kama huko waliko nako wenyeji wakiamua kuwafukuza baada ya kutambua
ubaguzi wao wataishije na wamenielewa,” alisema Mulongo.
Chanzo: Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment