Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
PSPF inter-college Bonanza Arusha lafana
Na Mwandishi Wetu,
Arusha
Bonanza maalum kwa ajili ya wanavyuo wa vyuo vya elimu ya
juu mkoani Arusha lililofanyika mwishoni mwa wiki (Mei 21, 2016)
Jijini Arusha lilifana, huku idadi kubwa ya wanafunzi wakijiunga na Mpango wa
Uchangiaji wa Hiari wa PSPF.
Viongozi wa vyuo
mbalimbali mkoani wakiwa katika picha ya pamoja Afisa Mfawidhi wa PSPF Arusha
Bw. Philbert Leina (wa tatu kutoka kushoto, mstari wa nyuma) baada kikao cha maandalii kilicho fanyika
katika ofisi za PSPF mkoa wa Arusha.
Tamasha hilo lililofanyika katika viwanja vya chuo cha
Uhasibu Arusha (IAA) kilichopo Njiro jijini Arusha, lilijumuisha vyuo vya
Makumira, Mt. Meru, SAUT, MAN U (Chuo Kikuu cha Arusha), Chuo cha Ufundi Arusha
na IAA.
Ukaguzi wa timu kabla ya
mchezo, wa tatu kulia ni Afisa Mfawidhi wa PSPF Arusha Bw. Philbert Leina.
Kwa upande wake Afisa mchezo wa Mkoa wa Arusha, alisema amefurahishwa sana kwa PSPF
kuandaa Bonanza hilo kwa wanavyuo wa mkoa wa Arusha na kuwataka wanavyuo
kuhakikisha mashindano yanaanza na kumalizika kwa usalama, lengo likiwa ni
kudumisha upendo na uhusiano Mwema kati ya vyuo hivyo.
Wanachuo wa IAA,
wakishangilia baada ya timu yao kuibuka mshindi katika mpira wa miguu.
Michezo iliyoshindaniwa ni pamoja na Football, Netball, Basketball na Volleyball,
hata hivyo mchezo uliovuta hisia za washiriki wengi ni mchezo wa mpira wa
miguu ambapo timu ya Chuo cha Uhasibu Arusha kilibuka mshindi
Wanachuo wa IAA,
wakishangilia baada ya timu yao kuibuka mshindi katika mpira wa miguu.
Michezo iliyoshindaniwa ni pamoja na Football, Netball, Basketball na Volleyball,
hata hivyo mchezo uliovuta hisia za washiriki wengi ni mchezo wa mpira wa
miguu ambapo timu ya Chuo cha Uhasibu Arusha kilibuka mshindi
Ukaguzi wa timu kabla ya
mchezo, wa tatu kulia ni Afisa Mfawidhi wa PSPF Arusha Bw. Philbert Leina.
Kwa upande wake Afisa mchezo wa Mkoa wa Arusha, alisema amefurahishwa sana kwa PSPF
kuandaa Bonanza hilo kwa wanavyuo wa mkoa wa Arusha na kuwataka wanavyuo
kuhakikisha mashindano yanaanza na kumalizika kwa usalama, lengo likiwa ni
kudumisha upendo na uhusiano Mwema kati ya vyuo hivyo.
Wawakilishi wa vyuo
vilivyoibuka washindi katika bonanza hilo wakiwa na katika picha pamoja na
Mgeni rasmi baada ya kukabidhiwa zawadi zao.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa mkuu wa Chuo cha Uhuasibu
Arusha, Bibi. Laura Kishala Aliishukuru PSPF kwa kuweza kuanda Bonaza hilo kwa
vyuo vya Arusha, akifafanua zaidi alisema, “Bonanza hili mliloliandaa hakika ni
jambo zuri sana kwa wanafunzi wetu kwani michezo ni afya, na pia tunashukuru
kwa elimu juu ya Mfuko wa PSPF, nina imani sasa wanafunzi wetu wamepata elimu
ya kutosha juu ya PSPF, “.
Pamoja na mashindano hayo, pia wanavyuo hao walipata
burudani kutoka kwa balozi wa PSPF Mrisho Mpoto, ambaye alikuwa na kikundi
chake cha sanaa. Mpoto alikuwa ni burudani tosha kwa wanavyuo hao.
Baada ya kupata elimu juu ya Mfuko, hususan katika Mpangowa
uchangiaji wa hiari (PSS), idadi kubwa ya wanavyuo hao walijiunga na mpango
huo.
0 comments:
Post a Comment