ZANZIBAR NA MKOA WA ARUSHA KUSHIRIKIANA KUKUZA SOKO LA UTALII KIMATAIFA


Na Pamela mollel, Arusha


Katika kukuza utalii hapa nchini,Zanzibar na Mkoa wa Arusha yaungana kukuza soko la utalii kimataifa na kutanua wigo kwenye eneo la Utalii wa Urithi,Utalii wa michezo na Utalii wa afya kupitia msimu wa kwanza wa Tamasha la Utalii na Uwekezaji Zanzibar utakaofanyika Oktoba 25-26 mwaka huu

Akizungumza na waandishi wa habari,katibu Mtendaji Kamisheni ya Utalii Zanzibar Aris Abbas Manji,anasema ujio wao Arusha ni kutangaza Tamasha hilo la utalii na uwekezaji kwa wadau wote wa utalii ili waweze kushiriki katika Tamasha hilo

Ameongeza kuwa Uchumi wa Zanzibar umekuwa ukichangiwa na sekta ya utalii kwa asilimia thelasini ambapo wameweza kutanua wigo wa bidhaa za utalii

Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh. Poul Makonda amepongeza ujio huo wa Tamasha la kwanza la utalii na uwekezaji Zanzibar,ambapo ameeleza kuwa Mkoa wa Arusha upo bega kwa bega na Zanzibar katika kuhakikisha wanachochea na kutengeneza mazingira mazuri katika sekta ya utalii ili kuwavutia Wageni wengi zaidi na kutoa ajira kwa vijana.




Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

REA YATUMIA BILIONI 15 KUSAMBAZA UMEME VITONGOJI 105 MKOA WA ARUSHA


MKUU wa Mkoa wa Arusha Mhe.Paul Makonda,akizungumza na wananchi wakati mara baada ya kumkabidhi Mkandarasi tenda atakayetekeleza mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji vya mkoa wa Arusha

 MKUU wa Mkoa wa Arusha Mhe.Paul Makonda,akizungumza na wananchi wakati mara baada ya kumkabidhi Mkandarasi tenda atakayetekeleza mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji vya mkoa wa Arusha



SEHEMU ya wananchi wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.Paul Makonda (hayupo pichani) ,akizungumza mara baada ya kumkabidhi Mkandarasi tenda atakayetekeleza mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji vya mkoa wa Arusha



SEHEMU ya wananchi wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.Paul Makonda (hayupo pichani) ,akizungumza mara baada ya kumkabidhi Mkandarasi tenda atakayetekeleza mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji vya mkoa wa Arusha



SEHEMU ya wananchi wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.Paul Makonda (hayupo pichani) ,akizungumza mara baada ya kumkabidhi Mkandarasi tenda atakayetekeleza mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji vya mkoa wa Arusha
Na.Mwandishi Wetu


MKUU wa Mkoa wa Arusha Mhe.Paul Makonda ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kazi nzuri ya kutekeleza miradi ya kusambaza umeme vijijini.

Mhe.Makonda ameyasema hayo jijini Arusha wakati wa kumtambulisha na kumkabidhi Mkandarasi atakayetekeleza mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji vya mkoa wa Arusha

Amesema kuwa miradi ya kusambaza umeme vijijini imewezesha wananchi kuunganishiwa umeme kwa gaharama nafuu na imeondoa dhana kuwa umeme ni wa matajiri.

Aidha amemtaka Mkandarasi aliyetambulishwa kutekeleza mradi huo kwa weledi na kwa kuzingatia muda wa mkataba aliopewa.

"Tunamtaka Mkandarasi kutekeleza mradi huo kwa uaminifu na hatutasita kuchukulia hatua pindi atakavyoshindwa kutekeleza kwa wakati na pia tunamtaka Mkandarasi kutumia vijana wetu waliopo katika mkoa wa Arusha kutekeleza mradi huo.

Naye Mkurugenzi wa umeme Vijijini REA, Mhandisi Jones Olotu,amesema kuwa jumla ya vitongoji 1,039 vitapatiwa umeme kupitia mradi huu.

"Vitongoji 105 kati ya 1,039 vilivyobaki vitapata huduma ya umeme kupitia mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji vyote nchini (HEP Densification project)."

Mhandisi Olotu alimtambulisha Mkandarasi anayetekeleza mradi huo ni kampuni ya CEYLEX ENGINEERING (Pvt) LTD na gharama ya mradi huo ni takribani shilingi bilioni 15 na utanufaisha wateja wapatao 3,465.


Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

CHUO CHA UHASIBU ARUSHA CHAUNGANA NA MATAIFA MENGINE KUADHIMISHA SIKU YA UTALII DUNIANI


Chuo Cha Uhasibu Arusha kwa kushirikiana na kampuni ya Rethinking Tourism Africa wamefanya kongamano la maadhimisho ya siku ya utalii duniani leo September 27,2024 kwa kushirikisha wadau wa sekta hiyo katika hoteli ya Gran Melia Jijini Arusha.

Akizungumza wakati wa kongamano hilo Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii mheshimiwa Dastan Kitandula amesema kuwa sekta ya utalii ina mchango mkubwa katika pato la taifa kwa asilimia 15.

Aidha amesema kuwa sekta hiyo pia inachangia fedha za kigeni kwa silimia 25 huku akisisitiza kuwa serikali inaendelea na mipango ya kufungua maeneo ya kusini mwa nchi ili kuendelea kukuza sekta hiyo muhimu kwa mustakabali wa Uchumi wan chi.

“Tunaendelea na Jitihada mbali mbali za kufungua maeneo mengine ambapo tunaelekea upande wa kusini na kuhakikisha pia tunateka masoko mengine ya kimataifa kwa sasa tayari tunafanya vizuri katika soko la Brazil,Asia,Marekani,Europe,China na India”Alisema Kitandula

Pia tutaendelea kuboresha Miundombinu ya Barabara na viwanja vya ndege ili kuhakikisha kuwa wanaotumia huduma hizo wanatumia mazingira rafiki na kufurahia huduma hiyo.

Kwa Upande wake Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha Profesa Eliaman Sedoyeka amesema kuwa chuo hicho ina vitivyo vitano ambapo ina kitengo kinachohusika na mambo ya Utalii hivyo kitengo hicho kwa kushikirikiana na wadau wameandaa kongamano hilo Arusha International Tourisms Conference an Expo ambalo lilianza rasmi mwaka 2023 na litaendelea kufanyika kila mwaka.

“Katika kongamano hili tunaleta wanazuoni na wadau mbali mbali kujadili muktadha mzima wa sekta ya utalii kuanzia masomo,utafiti,na hasa hususani katika soko,sasa sisi kama wadau kwa kuzingati utalii na biashara hii kinachouzwa ni Ujuzi mtu akija akiondoka aondoke na taswira nzuri ya nchi,sasa kwa kufanya hivyo rasilimali nis waka muhimu sana”alisisitiza sedoyeka.

Kutokana na hali hiyo amesema chuo hicho kinatoa mtaala wa shahada ya Utalii na uanagenzi ambapo wanafundisha wanafunzi kwa vitendo jinsi ya kuhudumia sekta hiyo kuanzia kupokea wageni mpaka uendeshaji wa sekta ya utalii kwa ujumla.

















Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

MAKAMU WA RAIS AWASILI MKOANI ARUSHA KUSHIRIKI KONGAMANO LA UHURU WA DINI LA AFRIKA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda wakati alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro akielekea mkoani Arusha leo tarehe 20 Septemba 2024.


Makamu wa Rais anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika Kuhitimisha Kongamano la Nne la Uhuru wa Kidini la Afrika litakayofanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha tarehe 21 Septemba 2024.





Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akisalimiana na Viongozi mbalimbali wakati alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro akielekea mkoani Arusha leo tarehe 20 Septemba 2024.


Makamu wa Rais anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika Kuhitimisha Kongamano la Nne la Uhuru wa Kidini la Afrika litakayofanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha tarehe 21 Septemba 2024.




Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN APONGEZA NSSF KWA KUFANYA MAGEUZI NA KUKAMILISHA MRADI WA KIWANDA CHA SUKARI MKULAZI


*Asema inatokana na NSSF kufanya mageuzi mbalimbali pamoja na kuwekeza vizuri kimkakati

Na MWANDISHI WETU,
ARUSHA. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameupongeza Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) na Jeshi la Magereza kwa kufanya mageuzi na kukamilisha mradi wa kimkakati wa kiwanda cha sukari Mkulazi kilichopo Mbigiri Mkoani Morogoro.

Amesema kukamilika kwa mradi huo wa kimkakati kunatokana na NSSF kufanya mageuzi mbalimbali ikiwemo kuwekeza kimkakati, kujipanga vizuri na kuusimamia vizuri mradi huo. Mradi wa kiwanda cha sukari Mkulazi ulizinduliwa rasmi Agosti 7, mwaka huu, una uwezo wa kuzalisha tani 50,000 kwa mwaka na tayari uzalishaji wa sukari ya majumbani ulianza tarehe 1 Julai, 2024.

Mhe. Dkt. Samia alitoa pongezi hizo tarehe 28 Agosti 2024 wakati akifungua kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa taasisi za umma kilichofanyika Mkoani Arusha.

“Nilipokuwa kwenye ziara Mkoani Morogoro nilifungua kiwanda cha sukari Mkulazi cha NSSF wakishirikiana na Jeshi la Magereza; hawa waliwekeza kimkakati, lakini wamefanikiwa baada ya kufanya mageuzi mbalimbali…hongereni sana NSSF,” amesema Mhe. Rais Dkt. Samia.

Aidha, alishauri kuwekeza kwa kufanya upembuzi yakinifu kwenye miradi mbalimbali ili iweze kuleta tija zaidi.

Akifunga kikao kazi hicho, Katibu Mkuu Kiongozi Dkt. Moses Kusiluka amesisitiza umuhimu kwa viongozi kutekeleza kwa ukamilifu maelekezo yote yaliyotolewa na Mhe. Rais Dkt. Samia wakati akifungua mkutano huo na kuwa Ofisi yake itahakikisha maelekezo hayo yanatekelezwa.

Dkt. Kusiluka pia amewataka wenyeviti na watendaji wakuu wa taasisi za umma kusimamia utendaji wa taasisi zao ili kuongeza ufanisi na tija hasa ukizingatia Serikali imefanya uwekezaji mkubwa kwenye taasisi hizo na inatarajia kupata manufaa kutokana na uwekezaji huo.

Aidha, ameiagiza Ofisi ya Msajili wa Hazina kutekeleza kikamilifu mfumo wa kupima ufanisi wa taasisi na mashirika ya umma kwa kuangalia matumizi sahihi ya rasilimali huku akisisitiza umuhimu taasisi zote kuhakikisha mifumo ya TEHAMA inasomana ili kurahisisha utendaji wa Serikali kufanyakazi pamoja.


WAHITIMU NELSON MANDELA WAASWA KUTOA HUDUMA BORA KWA JAMII

 

Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Balozi Maimuna Tarish akiongea na wahitimu na wageni waalikwa wakati wa Mahafali ya 10 ya Taasisi hiyo yaliyofanyika Agosti 29, 2024 Kampasi ya Tengeru Arusha.

.......

WAHITIMU 92 wa Shahada za Uzamivu na Umahiri kutoka Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela wameaswa kutatua changomoto katika jamii , sekta za uzalishaji pamoja na sekta ya huduma ili kuleta tija zaidi.

Hayo yalisemwa Agosti 29, 2024 Jijini Arusha na Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Taasisi hiyo. Balozi Maimuna Tarish wakati wa Mahafali ya 10 ya kutunuku wahitimu hao shahada za Uzamivu (PhD) na Umahiri (Masters).

"Naamini mtachangia katika kuleta maendeleo endelevu kama kauli mbiu yetu isemayo taaluma kwa jamii na viwanda iendelee kuwa mwanga na mwongozo katika maeneo yenu ya kazi"

Alisisitiza kuwa, mafanikio si kipimo cha yale unayojua bali ni namna unavyotumia kile unachokijua hivyo nendeni mkatumie maarifa na ujuzi mlioupata katika kujenga Tanzania na Bara la Afrika kwa ujumla.

Alisema, taasisi hiyo imejipambanua katika maeneo mbalimbali ikiwemo uhamilishaji wa teknolojia haswa katika ubunifu na utafiti unaozingatia maendeleo ya viwanda na changamoto za wananchi.

Alisema taasisi hiyo, imeendelea kutekelezeka mradi wa hosteli za kina mama wenye watoto wadogo na wanafunzi wenye mahitaji maalum ambapo sasa mradi huo umefikia asilimia 60 katika ujenzi wake.

Naye Mkuu wa Taasisi hiyo Prof. Maulilio Kipanyula alisema taasisi hiyo itaendelea kuwa kitovu cha maendeleo ya sayansi uhandisi, teknolojia na ubunifu katika ukanda wa Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Alisema mahafali hayo yana jumla ya wahitimu 92 kati yao wanawake ni 29 na wanaume ni 63 ambapo wahitimu 17 kati yao sawa na asilimia 18 ni wanafunzi wa kigeni kutoka nchi za Kenya, Ghana, Uganda, Burundi,Malawi ,Rwanda, Sudani Kusini na Nigeria.

Aliongeza kuwa kati ya wahitimu 64 walitunukiwa shahada mbalimbali za Umahiri huku wahitimu 28 walitunukiwa shahada za Uzamivu ambazo ni matunda ya kazi nzuri zinazofanywa na Shule Kuu Sayansi Uhai na Uhandisi Biolojia (LiSBE), Shule Kuu Sayansi ya Malighafi Nishati, Maji na Mazingira (MEWES) na Shule Kuu ya Hisabati, Sayansi na Uhandisi wa Ukokotoaji na Mawasiliano (CoSCE).

"Nashukuru Bodi ya Mikopo ya Elimu kwa kutoa mikopo kwa wanafunzi na wadau kutoka mashirika ya Maendeleo ikiwemo Beni ya Dunia, Benki ya Maendeleo ya Afrika , Serikali ya Ujerumani na wadau wengine kwa kuendelea kusaidia wanafunzi kwenye hatua mbalimbali za masomo yao " alisema Prof. Maulilio.

Prof. Gabriel Shirima Mlau wa Mahafali ya 10 ya Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela akiongoza maandamano wakati wa sherehe za mahafali Agosti 29, 2024 Kampasi ya Tengeru Arusha.

Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Bw. Omari Issa ( Katika mwenye Kofia nyekundu) akiwa na viongozi wa Taasisi wakati wa Sherehe za Mahafali ya 10 yaliyofanyika Agosti 29, 2024 katika Kampasi ya Tengeru Arusha.

Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Balozi Maimuna Tarish akiongea na wahitimu na wageni waalikwa wakati wa Mahafali ya 10 ya Taasisi hiyo yaliyofanyika Agosti 29, 2024 Kampasi ya Tengeru Arusha.

  

Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Bw. Omari Issa akiwatunuku Wahitimu Shahada ya Uzamivu wakati wa Mahafali ya 10 ya Taasisi hiyo Agosti 29, 2024 katika Kampasi ya Tengeru Arusha.

Wahitimu 92 wa Shahada ya Umahiri na Uzamivu kutoka Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela katika Mahafali ya 10 ya Taasisi hiyo Agosti 29, 2024 katika kampasi ya Tengeru Arusha.

Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Balozi Maimuna Tarish (Kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Makamu Mwenyekiti wa Baraza Prof. Lughano Kusiluka ( kushoto) wakati wa mahafali ya 10 ya taasisi hiyo Agosti 29, 2024 Kampasi ya Tengeru Arusha.


Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

MHANDISI SANGA AKAGUA ENEO LA SAMIA ARUSHA AFCON CITY


Na Munir Shemweta, WANMM

Katibu Mkuu wzara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga amekakagua eneo la Mradi wa Samia Arusha AFCON City (SAAC).

Eneo hilo lenye ukubwa wa ekari 4,555.5 lipo Kata ya Olmot na Olasiti katika Jiji la Arusha na limepakana na miradi miwili ya viwanja vitakavyotumika kwenye mashindano ya Afcon 2027.

Tanzania imepata fursa ya kuwa mwenyeji wa mashindano ya mpira wa miguu ya Mataifa ya Afrika yatakayofanyika mwaka 2027 ambapo tayari eneo litakalotumika kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa michezo hiyo limebanishwa.

Mhandisi Sanga ametembelea eneo hilo tarehe 28 Agosti 2024 jijini Arusha ikiwa ni jitihada zake za kuhakikisha mradi uliopangwa kutekelezwa kwenye eneo hilo unatekelezwa kwa wakati ambapo Wizara yake imelekeza eneo hilo kupangwa, kupimwa na kumilikishwa.

Kwa mujibu wa Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Arusha Geofrey Mwamsojo, eneo hilo likipangwa litawekwa huduma muhimu zitakazowezesha kuwa na mji nadhifu kulingana na matumizi yanayoendana na matumizi ya uwanja.


Amesema, Malengo ya mradi huo ni kuwa na mji nadhifu na himilifu na unaojitegemea wenye huduma zote wezeshi kwa uwanja wa michezo, kusaidia maendeleo ya Jiji la Arusha yanayofuata mpangilio bora wa makazi pamoja na kuongeza wigo wa viwanja vitakavyojengwa Hotel za kitalii kwa ajili ya Jiji la Arusha.

Mradi huo wa Samia Arusha Afcon City utatekelezwa kwa awamu tatu ambapo awamu ya kwanza ni utwaaji vipande vya ardhi pamoja na uthamini wa fidia ya vipande vya ardhi vitakavyoguswa na mradi, awamu ya pili kupanga eneo zima la mradi lenye ukubwa wa ekari 4555.5, Kupima eneo lenye ukubwa wa ekari 180 ili kugawa viwanja pamoja na Kufungua miundombinu ya barabara kuu na za ndani.


Awamu ya mwisho itakuwa endelevu na kuhusisha kazi za umilikishaji wa viwanja, maandalizi ya hati na vikao vya kamati ya ugawaji wa ardhi pamoja na usimamizi wa mradi utakao husisha utangazaji wa uuzaji wa viwanja vya mradi.

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga (Kulia) akipata maelezo kuhusiana na maendeleo ya utekelezaji mradi wa Samia Arusha Afcon City kutoka kwa Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Arusha Geofrey Mwamsojo (wa nne kushoto) alipokwenda kukagua utekelezaji mradi huo tarehe 28 Agosti jijini Arusha.

Muonekano wa eneo la Mradi wa Samia Arusha Afcon ambapo Wizara ya Ardhi inatekeleza kazi ya Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

Sehemu ya eneo la mradi wa Samia Arusha Afcon uliopo katika jiji la Arusha ambapo Wizara ya Ardhi inatekeleza kazi ya Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

RAIS SAMIA AFUNGUA KIKAO KAZI CHA WENYEVITI WA BODI NA WATENDAJI WAKUU WA TAASISI ZA UMMA JIJINI ARUSHA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwahutubia Viongozi mbalimbali kabla ya kufungua Kikao Kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) tarehe 28 Agosti, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama pamoja na viongozi wengine wakati wa Wimbo wa Taifa wa Tanzania na ule wa Afrika Mashariki ukiimbwa kabla ya kufungua Kikao Kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) tarehe 28 Agosti, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye Kikao Kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) tarehe 28 Agosti, 2024.
Viongozi mbalimbali, Wenyeviti wa Bodi pamoja na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma wakiwa kwenye Kikao Kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) tarehe 28 Agosti, 2024.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa