Arusha
Home » , , » NAIBU WAZIRI WA FEDHA KUFUNGUA MKUTANO MKUU GEPF ARUSHA

NAIBU WAZIRI WA FEDHA KUFUNGUA MKUTANO MKUU GEPF ARUSHA



Mkurugenzi mkuu wa mfuko Gepf , Daudi Msangi akizungumza leo na vyombo mbalimbali kuhusu, mkutano wa wadau wa mfuko huo ambao  utashirikisha wadau zaidi ya mia tatu kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini,,mgeni rasmi katika mkutano huo anatarajiwa kuwa  Naibu waziri wa fedha na mipango  Ashatu kijaja  kufungua mkutano  huo wa wadau wa mfuko wa mafao ya mstaafu (Gepf) utakaofanyika may 25 jijini Arusha.

Mwenyekiti wa bodi Ya wadhamini, Joyce shaidi akiongea na vyombo vya habari ambapo amesema kuwa, mfuko huo unatarajia kuwekeza kiasi cha kiasi cha shs bilioni moja na milioni mia sita katika kiwanda cha kutengeneza mashine cha Kilimanjaro machine tools kilichopo Mkoani kilimanjaro Kwa ajili ya kujenga kinu kidogo cha kufua vyuma.
Meneja masoko, Edgar shumbusho amesema kuwa, mfuko huo unalenga zaidi kutumia radio za jamii katika kuwafikishia wananchi wa vijijini elimu ambapo wamepata mafanikio makubwa Sana kupitia mfumo huo. 
Kushoto ni Meneja wa mfuko huo Mkoa wa Arusha,Clement Saning'o akifatia kwa ukaribu mkutano na waandishi wa habari 
 Meneja wa mfuko huo Magraret Mrina wa wilaya ya Ilala akijitambulisha kwa waandishi wa habari
 Kulia ni Afisa masoko wa mfuko huo wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Saalam akiteta jambo na Adam Hamza afisa masoko
Kushoto ni meneja kutoka mfuko huo Ramadhani Sossora kutoka Mbeya akifurahia jambo na mkurugenzi wa Key Media Arusha Sarah Keiya mara baada ya kumaliza mkutano na waandishi wa habari
 Meneja wa mfuko huo kutoka Mtwara Deogratias Kakoko akijitambulisha kwa waandishi wa habari
Naibu waziri wa fedha na mipango  Ashatu kijaja anatarajiwa kufungua mkutano wa nane wa wadau wa mfuko wa mafao ya mstaafu (Gepf) utakaofanyika may 25 jijini Arusha. 

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari, Mkurugenzi mkuu wa mfuko huo, Daudi Msangi amesema kuwa, mkutano huo utashirikisha wadau zaidi ya mia tatu kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini. 

Amesema kuwa,katika mkutano huo wanatarajia kujadili Mada mbalimbali ikiwemo kutoa elimu kwa wanachama pamoja na kuwasilisha taarifa za utendaji Kwa mwaka 2015/2016.

Msangi ameongeza kuwa, ndani Ya siku hizo mbili za mkutano mbali na kujadili taarifa za wanachama wanatarajia kutoa misaada wa mashuka Kwa watoto na wanawake wajawazito katika hospital ya dareda iliyopo wilayani babati Mkoani Manyara. 

Hata hivyo ameongeza kuwa, mfuko huo umekuwa ukitoa misaada Kwa kuangalia mahitaji ya jamii popote nchini na kuweza kusaidia kulingana na mahitaji hayo. 

Mwenyekiti wa bodi Ya wadhamini, Joyce shaidi amesema kuwa, mfuko huo unatarajia kuwekeza kiasi cha kiasi cha shs bilioni moja na milioni mia sita katika kiwanda cha kutengeneza mashine cha Kilimanjaro machine tools kilichopo Mkoani kilimanjaro Kwa ajili ya kujenga kinu kidogo cha kufua vyuma. 

Amesema kuwa,uwepo wa kinu hicho utasaidia kuinua uzalishaji wa kiwanda hicho, huku kwa sasa watawekeza kinu kidogo ambapo kwa baadaye wataendelea na kuwekeza kinu kikubwa. 

Kwa upande wa meneja masoko, Edgar shumbusho amesema kuwa, mfuko huo unalenga zaidi kutumia radio za jamii katika kuwafikishia wananchi wa vijijini elimu ambapo wamepata mafanikio makubwa Sana kupitia mfumo huo. 

Ameongeza kuwa, mfuko huo umekuwa ukitoa mafao mbalimbali ikiwemo fao la msaada wa mazishi Kwa wanachama wake, na sambamba na kutoa elimu kwa watoto wa wanachama. 

Aidha kauli mbiu Ya mkutano huo ni hifadhi ya jamii kwa wote inawezekana katika uchumi wa viwanda.


Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa