Arusha
Home » » Walioficha sukari ardhi iwakatae

Walioficha sukari ardhi iwakatae

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 




Na: Lilian Lundo – MAELEZO


Askofu wa Kanisa la Good News for All Ministry Dkt. Charles Gadi amewapa siku tatu walioficha sukari kuitoa na ikiwa watakaidi agizo hilo basi ardhi iwakatae.

Askofu Gadi ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya uhaba wa sukari nchini na  maandalizi ya mkutano wa kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania utakaofanyika jiji la Arusha.

“Tanzania haina tatizo la sukari bali sukari ziko kwenye maghala, wafanyabiashara wamezificha ili waje kuuza kwa bei ya juu. Tunamuomba Mungu ili watu hao ardhi iwakatae ikiwa hawatatoa sukari ndani ya siku ya tatu,”alisema Askofu huyo.

Pia, Askofu Gadi ametoa wito kwa wafanyabiashara kuacha tabia ya kuficha sukari na wakumbuke kuwa waislam wapo katika maandalizi ya kutimiza nguzo muhimu ya imani ya dini yao ambapo wataanza  mwezi wa Ramadhani na watahitaji sukari kwa ajili ya kuandaa futari.

Vile vile Askofu huyo ameiomba Serikali kuagiza sukari kwa wingi ili waumini wa dini ya Kiislam waweze kutimiza kwa urahisi nguzo ya mwezi wa Ramadhani.

Aidha, akizungumzia juu ya mkutano wa maombi utakaofanyika jiji la Arusha, Askofu Gadi amesema kuwa mkutano huo ni maalum kwa ajili ya kumuombe Rais Dkt. John Pombe Magufuli ili aweze kufanikiwa katika nia yake ya kujenga upya uchumi, uadilifu na ustawi wa Tanzania.

Mkutano huo unategemewa kufanyika siku ya Jumatano Juni 08, 2016 kuanzia 4 asubuhi mpaka saa 12 jioni viwanja vya relini, ambao umeandaliwa na Kanisa la Good News for All Ministry kwa kushirikiana na Umoja wa Makanisa ya Arusha.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa