by mbuya Godfriend
Mjumbe wa kamati kuu ya Chadema na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa
amewataka watanzania kuwa na imani na Chadema kwa kuwa maeneo
yanayoongozwa na chama chichokatika halmashauri na majimbo yana
maendeleo tofauti na maeneo mengine.
kata ya Moita Bwawani ambapo pamoja na mambo mengine amewashukuru wananchi waliompigia kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
''Wanakuja Simanjiro, Kiteto, Ngorongoro, Longido hawatuwezi na
wakitaka waje maeneo haya walinganishe na maeneo yao hawatuwezi,
ninawashukuru sana kwa kuhama na mimi toka CCM kwenda Chadema''-Amesema
Lowassa.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Salum Mwalimu amesema
chama chao siyo chama cha upembuzi yakinifu na urasimu bali chama chao
ni chama cha kufanya kazi kwa vitendo ambapo watahakikisha wanapeleka
maji eneo la Moita Bwawani.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Monduli Isack Joseph amewataka watendaji
na wenyeviti wa vijiji kutokuruhusu wakandarasi kufanya kazi bila wao
kupata barua na kujirishisha na miradi itakayotekelezwa na kuhakikisha
wanaisimamia ili iwe na tija kwa wananchi
0 comments:
Post a Comment