Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
CHAMA cha Walimu Tanzania (CWT) wilayani Arumeru, kimeomba serikali
kuharakisha malipo ya malimbikizo ya madeni yanayofikia Sh milioni 800
katika wilaya hiyo ili kuwawezesha walimu kufanyakazi kwa kasi zaidi.
Aidha, chama hicho jana kiliwaaga walimu wastaafu 31 wilayani humo na
kuwapatia zawadi ya mabati 620, kila mmoja akipata mabati 20 kama
kumbukumbu ya utumishi wa ualimu nchini.
Akizungumza jana wakati wa hafla ya kuwaaga waalimu hao, Katibu wa
CWT wilayani Arumeru, Joyce Kijazi, alisema serikali ikiharakisha kulipa
madeni ya walimu, itahamasisha utendaji kazi ulio bora zaidi.
Aliiomba serikali kuharakisha ulipaji wa madeni hayo yaliofikia Sh
milioni 800 kwa wilaya hiyo, fedha ambazo ni mapunjo ya mishahara,
mishahara ya nyuma, fedha za uhamisho, matibabu, mazishi na masomo.
Kijazi alisema madeni hayo ni malimbikizo ya tangu mwaka 2009. Kuhusu
walimu waliostaafu, alisema zawadi hiyo ya mabati 20 kwa kila mmoja ni
moja ya utekelezaji wa agizo lililotolewa katika mkutano mkuu wa CWT
Taifa, uliokaa mwaka 2014 na kuazimia kuwapatia mabati 20 kwa kila
mwalimu atakayestaafu kuanzia kipindi cha Julai 2015.
Walimu hao 31 walistaafu kati ya Julai na Septemba mwaka jana.
CHANZO: GAZETI LA HABARI LEO.
0 comments:
Post a Comment