Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
KAMATI ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Kilimanjaro, ikiongozwa na Mkuu
wa Mkoa huo, Amos Makalla, imetekeketeza pombe haramu ya gongo lita
140, mitambo sita na mapipa 33 yenye malighafi ya kutengenezea pombe
hiyo, katika Kijiji cha Kikelelwa wilayani Rombo.
Akizungumza wakati wa kuteteketeza pombe hiyo, Makala alisema
Wilaya ya Rombo inaongoza kwa kutengeneza pombe za kienyeji zaidi ya 50
kwa kutumia kemikali ambazo ni hatari kwa afya za binadamu.
Alisema kemikali zinazotumika kiutengeneza pombe hizo haramu ni
pamoja na mbolea ya urea, kinyesi cha binadamu, unga wa betri, sukari
guru na molasesi.
“Hii ni hatari ndugu zangu hatuwezi kujenga Taifa kwa njia hii, pombe
haramu haikubaliki na hupoteza nguvu kazi ya Taifa, leo tumetekeza
pombe hizi na kazi hii itakuwa ya kudumu na vyombo vya ulinzi vipo macho
wakati wote.
“… wale watakaobainika kuendelea na biashara hii ya pombe haramu
pamoja na mambo mengine ambayo ni kinyume cha sheria, watatiwa mbaroni
tu,” alisema Makalla.
Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho kilichopo mpakani mwa
Tanzania na
Kenya, walisema utengenezaji wa pombe hiyo imeleta madhara makubwa kwa
wananchi wa Rombo hususan vijana hali ambayo inasababisha wanawake wengi
kubeba mzigo wa kuhudumia familia.
Ofisa Mtendaji wa Kata ya Tarakea Motamburi, Nicodemas Kimaro,
alisema kazi ya ukamaji wa pombe haramu ilianza Januari mwaka huu.
“Pamoja Serikali kupiga marufuku utengenezaji wa pombe haramu zote
ikiwamo gongo lakini bado kuna baadhi ya watu wamekuwa wakikaidi amri
hii,” alisema Kimaro.
CHANZO,GAZETI LA MTANZANIA
0 comments:
Post a Comment