JenikisaNdile
– MAELEZO
10/09/2015.
Dar es salaam.
Wizara ya Elimu na Mafunzo
ya Ufundi imeandaa Kongamano la siku mbili la Elimu ya Juu litakalofanyika jijini
Arusha kwa lengo la kuwa na jukwaa la kubadilishana uzoefu na maarifa miongoni mwa
wadau wa elimu nchini.
Hayo yamesemwa na Katibu
Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) Prof. Yunus Mgaya alipokuwa akizungumza
na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam .
Amesema Kongamano hilo litaenda
sambamba na Maonesho ya shughuli mbalimbali zikiwemo za utoaji wa huduma, na
maonesho ya bidhaa mbalimbali kuonyesha mafanikio ya elimu yaliyopatikana nchini.
Amesema washiriki wa
mkutano huo kutoka taasisi mbalimbali watapata fursa ya kuchangia miradi elimu kwa
ili kuinua sekta hiyo hapa nchini.
“Tunatarajia kuweka mikakati
itakayowezesha kuwa na ushirikiano madhubuti baina ya Taasisi za Elimu ya Juu na
Sekta Binafsi ili kubaini fursa na changamoto zilizopo tukilenga kuchochea maendeleo
na kukuza ajira kwa wahitimu wetu ”, Alisema Prof.Mgaya.
Amefafanua kuwa Kongamano
hilo la siku mbili litafanyika mnamo tarehe 1 hadi 2 Oktoba2015 katika Hoteli ya
Naura Springs jijini Arusha likiongozwa na Kauli Mbiu isemayo “Kujenga Uwezo kwa ajili ya
uzalishaji na ushinda ni Kitaifa :Matarajio na changamoto kwa muongo ujao”.
Wizara ya Elimu imeandaa kongamano hilo kwa kushirikiana
na Tume ya Vyuo Vikuu (TCU), Baraza la Taifa la Elimuya Ufundi (NACTE) Kamati ya
Makamu wa Vyuo Vikuu nchini (CVCPT) pamoja na wadau wa Elimu ya Juu kutoka ndani na nje nchi, Watendaji wa Serikali,
Sekta Binafsi, Wabia wa Maendeleo, Taasisi zisizo za Kiserikali, Vyama vya Kitaaluma,
Wahadhiri, Chama cha WaajirinaWanasiasa.
0 comments:
Post a Comment