Arusha
Home » » WALIMU ARUSHA WAIDAI SERIKALI BILIONI 4

WALIMU ARUSHA WAIDAI SERIKALI BILIONI 4

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mwenyekiti wa Chama cha Walimu mkoa wa Arusha ,Mwalimu Jovin  Kuyenga
akizungumza na waandishi wa habari jana Ofisini kwake  juu ya deni la
shilingi bilioni 4 wanalodai  kwa serikali,kushoto ni Katibu wa Chama cha
Walimu mkoa wa Arusha, Mwalimu Hassan Saidi.
 
]Na Woinde Shizza,Arusha

Chama cha Walimu mkoa wa Arusha CWT wamelalamikia serikali na kuitaka
kutekeleza kwa wakati madeni yao la zaidi ya billioni 4 kwani yamekuwa
kikwazo katika ufanisi wa kazi hali ambayo inapelekea walimu wengi
kushindwa kuendelea kufanya kazi kwa moyo na kujituma jambo ambalo linaweza
kushusha kiwango cha elimu nchini.

Akizungumza na Waandishi wa habari, Mwenyekiti wa chama cha walimu mkoa wa
Arusha Mwalimu Juvin Kuyenga amesema, kumekuwa na chanagamoto kubwa ambazo
zinakwamisha ufanisi wa kazi kwa walimu kwani wanazidai halmashauri
zilizopo mkoani zarusha zaidi ya billioni nne ,amabapo katika jiji la
arusha wanadai millioni  987,689,00,Arumeru billioni
2,996,607,848.21,Karatu  millioni 423,983,820,Longido millioni 171,112,680,
Ngorongoro million 169,000,000, na Monduli 135,832,000.
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa