Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Askofu Mkuu wa Kanisa la International Evangelism Church
Eliud Isanja (wapili kushoto) akiwa katika mahafali ya chuo cha Bibilia
kinachomilikiwa na kanisa hilo.watatu kushoto ni Mgeni Rasmi Kwa upande
wake Askofu Mwangalizi wa Kanisa hilo Israel Maasa
Na woinde shizza ,Arusha
Eliud Isanja (wapili kushoto) akiwa katika mahafali ya chuo cha Bibilia
kinachomilikiwa na kanisa hilo.watatu kushoto ni Mgeni Rasmi Kwa upande
wake Askofu Mwangalizi wa Kanisa hilo Israel Maasa
Na woinde shizza ,Arusha
Askofu
Mkuu wa Kanisa la International Evangelism Church Eliud Isanja
amewataka Watanzania wajitokeze kwa wingi kujiandikisha katika daftari
la kudumu la wapiga kura ili kutimiza haki yao ya kikatiba na kuchagua
viongozi bora watakaoleta maendeleo ya taifa.
Isanja
aliwaasa Watanzania kutozembea nafasi hiyo muhimu na badala yake
waitumie fursa hiyo itakayoleta mabadiliko yanayotarajiwa na wengi.
Akizungumza
katika mahafali ya Wahitimu wa Diploma ya masomo ya Biblia amesema kuwa
Tanzania inahitaji Viongozi waadilifu na wenye bidii. “Watu wasipige tu
kelele barabarani bali wajitokeze kwa wingi kujiandikisha na kupiga kura ili kupata viongozi bora watakaoliongoza taifa hili” Alisema Isanja
Kwa
upande wake Askofu Mwangalizi wa Kanisa hilo Israel Maasa ambaye alikua
mgeni wa heshima katika mahafali hayo amewataka watanzania kuwa makini
na wagombea wanaowagawa Watu kwa misingi ya ukabila na udini na
kutowachagua kwani wataathiri umoja na mshikamano wa kitaifa.
Wilfred
Pallangyo ameeleza kuwa ni wakati wa Watanzania kuwatambua viongozi
watakaofaa kuliongoza taifa na kuwapa nafasi hiyo pasipokufanya makosa
pia kuepuka vitendo vya rushwa hasa tunapoelekea katika uchaguzi mkuu.
Alisema
kuwa Tayari zoezi la uandikishaji limeanza katika baadhi ya mikoa na
linategemewa kukamilika nchini kote ili kukamilisha uchaguzi utakaoanza
Octoba mwaka huu,vuguvugu la uchaguzi tayari limeanza tumeshuhudia
hekaheka za wagombea wa Urais.
0 comments:
Post a Comment