Arusha
Home » » WANAWAKE NA VIJANA ARUSHA WAKABILIWA NA TISHIO LA KANSA YA NGOZI

WANAWAKE NA VIJANA ARUSHA WAKABILIWA NA TISHIO LA KANSA YA NGOZI


Mkoa wa arusha unaendelea kukabiliwa na ongezekao la uingizaji  na utumiaji wa vipodozi vyenye kemikali za sumu na vilivyopita  muda wa matumizi tatizo linaloendelea kutishia afya za wanawake  na vijana  kupata  magonjwa  ya  kansa  ikiwemo ya ngozi.
Akizungumza baada ya mamala ya chakula na dawa kukamata tani mbili za vipodozi vyenye viambata vya sumu na vilivyopita muda  wa matumizi katika maduka mbalimbali ya jiji la arusha afisa  afya  wa jiji hilo Bi. Anjela Mhitu amesema kama hali hiyo haitadhibitiwa na vijana na  wanawake  hawatawezeshwa  kuepuka janga hilo wengi wataangamia. Meneja wa mamlaka ya chakula na dawa kanda ya kaskazini Bw.Damas  Matiko amesema shehena ya vipodozi walivyokamata ina thamani ya milioni saba na pamoja na jitihada wanazofanya tatizo bado ni  kubwa na amewaomba wadau wa sekta za afya kusaidia tatizo hilo  kwa kudhibiti na kutoa elimu ya madhara yanayoikabili  jamii kama ikiendelea kutumia bidhaa  hizo. Mmoja wa watuhumiwa waliokutwa na bidhaa hizo amesema bidhaa  zilizokamatwa zilikuwa zimechanganywa ndani ya kontena la bidhaa halali na amekamatwa wakati anazichambua ili akaziharibu   maelezo ambayo hata hivyo yamepingwa vikali na maafisa wa TFDA.
Chanzo:ITV Tanzania
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa